Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

SEMINA YA UJASIRIAMALI NDANI YA NCHI YA AHADI NA MCH. HARRIS KAPIGA.





MCH. HARRIS KAPIGA.
Wakati wengine wanatumia uwezo wa fursa ama elimu walizo nazo kujipatia kipato kwa wale wenye kuhitaji ujuzi wa kitu fulani, Ndani ya huduma ya NCHI YA AHADI, Sinza Kamanyola kuna semina na mafunzo ya ujasiriamali na yanatolewa bure bila malipo yeyote na ni kwa watu wa aina zote kwa maana ya watu wa Imani zote.

Jana tar. 12 Jan 2013 Blog hii ilifanikiwa kuhudhuria Semina hii. Ki ukweli ilikuwa nzuri sana pia kulikuwa na shuhuda nzuri sana za jinsi mtu alivyoweza KUTHUBUTI (Daring).

Abela na Robert (mkurugenzi) walikuwa wazungumzaji!


Abela akiwa anagonga nyundo.

Dada Abela alizungumzia takribani mambo matano ya msingi, somo lilibeba kichwa kisemacho '' JINSI YA KUJIENDELEZA KIFANI ''_ How can we develop our carrier!

1. TAMBUA KUSUDI LAKO DUNIANI.
2. MAONO YAKO DUNIANI NI NINI
3. UNAPENDELEZ NINI (VALUES/INTERESTS)
4. UNA HAIBA YA AINA GANI (PERSONALITY)
5. ANGALIA FURSA ZAKO (EXPLORE YOUR POSSIBILITIES)

Hivyo ni vidokezo tu (highlights) ya vile alivyofundisha na alifafanua kwa kina sana.

Robert naye aliachilia nyundo zake!

Alizungumzia mambo makuu ya msingi. Sitatoa maelezo bali nakupa dondoo tu ya kile alichozungumza. Ukitaka ufaidi vizuri unakaribishwa NCHI YA AHADI, Sinza Kamanyola; DSM

DONDOO/HIGHLIGHTS
1. KUJIAMINI
2. KUJIZUIA/KUWA NA NIDHAMU
3. UVUMILIVU.


Rose Tarimo alitoa ushuhuda wenye kujenga sana sio kusisimua!


Dada Rose Tarimo ni moja kati ya watu ambao wanastahili kufuatwa as a role modal. Huyu dada baada ya kumaliza elimu ya msingi alikaa nyumbani miaka nane lakini ndani yake alikuwa na shauku kuu ya kutaka kusoma wakati huo hana mtu wa kumsomesha!
Aliamua kukusanya madaftari ya wanafunzi wa sekondari na kuanza kujisomea mwenyewe bila ya mwalimu, baadae akanunua namba ya mtihani. Akafanya mtihani akapata Division 1. akaenda kidato cha tano na sita hatimaye Chuo kikuu cha Dodoma na sasa ana degree. 
NI KWA SABABU ALITHUBUTU.

ALIZUNGUMZIA MAMBO MATATU YANAYOWEZA KUMTOA MTU KUTOKA SEHEMU MOJA HADI NYINGINE NA NDIO MAMBO YALIYOMTOA YEYE (ROSE)

1. DESIRE (SHAUKU KUU)
2. DETERMINATION (DHAMIRIO/KIU)
3. FAITH (IMANI)

Walihudhuria watu wa dini/imani tofautitofauti na ndio kusudio la semina hizi.


ANGALIA PICHA MBALI MBALI.






















MUNGU AKUBARIKI, USIKOSE KUFIKA NCHI YA AHADI.
MCH. HARRIS KAPIGA ATAKUWA AKITOA RATIBA ZAIDI KILA SIKU YA JUMAPILI KWENYE KIPINDI CHA GOSPEL TRACK (G.T) AMBACHO KINAENDESHWA NA YEYE MWENYEWE KUPITIA CLOUDS FM RADIO.


KUMBUKA: 
Kama ambavyo Blog hii imekuwa ikikuletea mafundisho yenye kubadilisha ufahamu/akili na maisha kwa ujumla; Unaweza kui-support Blog hii kwa kununua mafuta halisi ya alizeti yenyo ubora wa juu, Lengo ni kufanikisha Blog hii Iendelee kukuletea mafundisho mazuri kutoka kwa watu maarufu na waliofanikiwa ambao nimekuwa nao bega kwa bega ili kuhakikisha msomaji wangu anapata kitu kitakachoweza kumtoa hatua moja kwenda hatua nyingine!
   Ili kujipatia Mafuta haya waweza kuwasiliana nasi kwa  0659 700 002 na Mungu atakubariki.
Asanteni sana wadau wangu! 


GH


DREAM BIG AS YOU GROW BIG

Mawasiliano:

+255 659 700 002
+255 756 145 417
mdeejunior@gmanil.com
mdee.junior (skype)
@mdee_junior (twitter)




Juu