Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

TUNAJIFUNZA NINI KWA MWEREZI WA LEBANONI ?

By Rev. Meinrald Anthony Mtitu.















Bonyeza hapa ununue mafuta halisi ya alizeti yasiyochakachuliwa kutoka Singida ili ku-support Blog hii.

Psalms 92:12-15
Key verse 12b.  Atakuwa kama mwerezi wa Lebanoni

Kabla ya kutambua ni nini hasa ambacho Mungu anapenda tujifunze kwa mwerezi, ni lazima kwanza tutambue sifa za mwerezi halafu ndipo tunaweza kuyaingiza maisha yetu humo kama kanisa la Tanzania (mwili wa Kristo) na mtu mmoja mmoja!



SIFA ZA MWEREZI WA LEBANONI
1. Unavutia
2. Mrefu sana, unakadiriwa kuwa na urefu kati ya mita 40-45
3. Matawi yake yamesheheni majani
4. Una mzunguko (circumference) wa mita 11-12
5. Unaishi miaka mingi (approx. 1000-2000 yrs)
6. Unaweza kustahimili misimu yote ( all seasons ) na majani yake hayapukutiki.
7. Una mizizi mirefu sana kwenda chini hivyo haung'oleki kirahisi.
8. Hauozi: kwa sababu hakuna mdudu yeyote anayeweza kuula, una harufu ya asili ambayo
    hufukuzawadudu wa aina zote.

Mwerezi ni picha ya Uimara na Uthabiti.

TUNAJIFUNZA NINI KWA MWEREZI

1. Mungu anatutaka tukue kwenda chini.
    Kabla ya kwenda juu sana lazima uende chini kwanza (Ukuaji)

Aina za Ukuaji
a, Ukuaji wa kwenda chini
b, Ukuaji wa kwenda juu.

Ukuaji wa kwenda chini.
Ili tuwe hivyo ni lazima tuwe na mizizi kwa sababu ndio inayosafirisha nishati(minerals) pia hutafuta Uhai. Katika hili ndiko tunajenga mambo ya msingi yafuatayo:

Ukuaji wa kiroho
> Ukuaji wa uhusiano wetu na Mungu yaani kutafuta source yetu na Mungu.
> Uhusiano wetu na Mungu ndio unaoleta maendeleo ya ukuaji wetu
> Mizizi ya kiroho.

Kukua kwenda juu.
Haya ni maisha yasiyofichika ambayo watu wengine watayaona ( Ushuhuda )


2. Mungu anataka tukue kwa nje/kupanuka (outward growth)
    Ni maisha ya kuongezeka katika kuwa baraka kwa watu wengine.

3. Mungu anataka tuwe na ukuaji endelevu (onward growth)
    Hubaki kuwa wa ukijani misimu yote (remain evergreen in all seasons)
    Hauchoki/haukomi kukua

Tusikome kukua katika Mungu.

Asante kwa kuwa pamoja nami, AMEN!






Juu