Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

Fundisho La Msingi I NENO LA MUNGU NI NINI NA SIO NINI...

   http://mdeejunior.blogspot.com     Kutokufahamu maana halisi ya Neno la Mungu kumeleta tatizo kubwa kwa Wakristo wengi kama sio wote kuishi kwa mazoea na kumuwekea Mungu mipaka ya kiutendaji! Naomba tuingie kwenye somo. 
   Bwana Yesu husika na kila mmoja anayeenda kujifunza hiki ambacho unamletea siku ya leo, fungua fahamu na moyo wa kupokea; kwa Jina lako Yesu, Amen!





Neno la Mungu sio nini:


> Neno la Mungu sio Historia ya Mungu.

> Neno la Mungu si-habari kuhusu Mungu.
> Neno la Mungu si-mapokeo ya kidini.

Neno la Mungu ni nini:


Neno la Mungu ni NIA / AZIMIO ndani ya moyo wa Mungu na ni kama mawazo. Lakini Mungu anapoitamka / anapoisema nia yake - Hilo ni Neno la Mungu. Neno la Mungu ni NIA iliyosemwa na Mungu.


Mithali 23:7a

Maana aonavyo mtu nafsini mwake, ndivyo alivyo.

* Awazavyo mtu ndivyo alivyo.
* Ukifanikiwa kuyakamata mawazo ya mtu fulani, utakuwa umemkamata mtu huyo.
* Nafsi ya mtu ni jumla ya mawazo awazayo.

Mungu na wazo lake ni mtu mmoja, yaani vile Mungu awazavyo ndivyo alivyo. Mungu ana uwezo.

Zaburi 33:6, 11
Kwa neno la BWANA mbingu zilifanyika, Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.
Shauri la BWANA lasimama milele, Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi.
* Hili neno liko juu ya historia na habari ya Mungu.

Yohana 1:1 
''Naye Neno alikuwa Mungu''

> Muundo mzima wa mawazo ya mtu, ndivyo mtu huyo alivyo; na ndivyo ilivyo hata kwa Mungu.

> Moyo wa Mungu ndio Mungu mwenyewe.

Marko 7:1-9
' Kisha Mafarisayo, na baadhi ya waandishi waliotoka Yerusalemu, wakakusanyika mbele yake, wakaona wengine katika wanafunzi wake wakila vyakula kwa mikono najisi, yaani, isiyonawiwa. Kwa maana Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao...'

> Tunaona wazi kabisa, hapa wanafunzi walikuwa wakibomoa historia na mapokeo ya kidini.
Mfano: Nyoka wa shaba pale jangwani > Nia ya Mungu ilikuwa ni kutoa unabii juu ya Yesu Kristo. Yesu Kristo akapambana na Mafarisayo na Wayahudi ili kuwatoa katika historia ya Musa na kuwaingiza katika NIA ya Mungu.

Maombolezo 3:33. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.
> Uzima uko ndani ya Neno la Mungu.

Luka 12:13-15
Mtu mmoja katika mkutano akamwambia, Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie urithi wetu. Akamwambia, mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu? Akawaambia, angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.

> Yesu anajua ukweli wote, hakuna uzima katika wingi wa vitu.
> Uzima - ni furaha, amani, na upendo ndani ya mioyo yetu.
Uzima unapatikana wapi kama sio katika wingi wa vitu? Yohana 1:1,4- uzima unapatikana ndani ya neno la Mungu.

Zaburi 23:1.
Bwana ndiye Mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Hapa Daudi alikuwa anamaanisha hivi:
* Ndani ya Mungu nimejaa kila kitu.
* Nimejaa furaha, shangwe, uzima, amani, - mtu awaye yote asinisumbue.
* Shetani anawadanganya watu kwa sababu wamekata tamaa katika umaskini.
> Ili kuwa na furaha na ujasiri kama wa Daudi ni lazima KUJAA.
> Mtu aliyejaa huwezi kumwonea huruma; mfano. Yesu hawakumuonea huruma, maana ALIJAA.
> Ili Mungu aweze kukutana na mahitaji yetu ni lazima tuwe na charge / TUJAE.

Yakobo 1:2-4
Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbali mbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.

> Hii ni hatua ya KUJAA.
> Saburi hutufanya kuwa watimilifu na utimilifu huo kuwa mkamilifu.
> Ni lazima kukaza moyo. Pasipo kukaza moyo huwezi kuyaona hayo.

Habakuki 3:17-19
Maana mtini hautachanua maua, wala mizabibuni hamtakuwa na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, na mashamba hayatatoa chakula; zizini hamtakuwa na kundi, wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng'ombe; Walakini nitamfurahia Bwana, nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu. Yehova, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.

Naomba maoni yako humu.

Dream Big As You Grow Big

By. mdee junior.

Contact:

+255 659 700 002
+255 756 145 417

mdeejunior@gmail.com (email)

@mdee_junior (twitter)
mdee.junior (skype)







Juu