Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

KUKUA KIROHO (SPIRITUAL LEVELS) NA SAM SASALI a.k.a Papaa NDANI YA NCHI YA AHADI JUMAPILI YA LEO.

Ze blogger Sam Sasali, Papaa leo alishusha nondo za ukweli kama sio misumari ndani ya huduma ya Nchi Ya Ahadi iliyo chini ya mchungaji kiongozi Harris Kapiga, Sinza Kamanyola; Dsm.

Andiko lililokuwa limebeba ujumbe mzima lilitoka kwenye kitabu cha Wagalatia 4:1...
''Mrithi awapo mtoto hana tofauti na mtumwa ingawa ni bwana wa wote''. Atakuwa chini ya uangalizi mpaka wakati ulioamriwa na baba (Mungu).
* Ishu hapa sio kwamba urithi haupo la hasha ila ishu ni kwamba Mrithi ni mtoto na mrithi akiwa mtoto ni sawa sawa na mtumwa.
* Tatizo sio kwamba Mungu hajatupa ahadi bali tatizo ni level / viwango katika kuiendea ahadi.
* Kila mtu anapewa kulingana na level aliyo nayo.

1Sam 17:16-17.  Kuomba vibaya sio yale maneno unayoongea mbele za Mungu bali NIA uliyo nayo juu ya kile unachoomba kwa Mungu.
* Unapokaa vizuri na Mungu hata level yako ya kukua inaongezeka.
* Hatumjui Kristo kwa kuimba mapambio.
* Shetani hana haja/agenda na mimi au wewe bali ana agenda na kile ulicho nacho / kile kilicho nyuma yako ambacho kinaweza kukupeleka level nyingine.
* Shetani hakuwa na agenda na Adamu au Eva bali kile walichokuwa nacho; alilenga kile walichokibeba. Adamu alipewa agizo asile tunda hivyo agenda ya shetani ilikuwa ni lile agizo alililopewa Adamu na Mungu.
* Yesu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea, kilichopotea hapa sio mtu bali ushirika kati ya mtu na Mungu (fellowship).

MAENEO YA KUONGEZA LEVEL / VIWANGO.

Mfalme yule alitoa talanta kwa kila mjoli wake kulingana na level / uwezo wa kila mtu.
Ugomvi wa Mungu na mwanadamu ni UTII / OBEDIENCE.

1. Kulifahamu / kulisikia na kulijua Neno la Mungu.
Mungu huzungumza kupitia Neno lake.
Level au uwezo ulio nao lazima utofautiane na yule anayeokoka leo. Kila mtu anakua (growth) kutokana na level aliyo nayo.

* Yesu anapotoa mwaliko ''njooni kwangu nyote wenye kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha'' Swali linakuja, je! nini kinafuata baada ya kupumzika?
Hahahhaaa ts funny, Baada ya kupumzika unakuwa umepata nguvu mpya za kukuwezesha kubeba mizigo yako uliyo nayo na kuendelea na safari yako kwani utakuwa na nguvu za kubeba hiyo mizigo/ jaribu ulilo nalo mara baada ya kupumzishwa na kujifunza miguuni kwa Yesu jinsi ya kuendelea na safari. Maana asema hivi; mjifunze kwangu, hivyo kuna shule ya kujifunza hapo kwa sababu Yesu hajasema njooni mniachie mizigo yenu bali njooni niwapumzishe then mwendelee na safari yenu.
* Ukristo ni mchakato endelevu. / Continuous Process. Lazima tukue katika kulisoma Neno la Mungu.

2. Maombi (sio maombezi).
* Watu wengi wanaopenda maombezi hawana Neno ndani yao. Mtu mwenye Neno / aliyejaa Neno ana maneno mengi ya kumwambia Mungu kwa sababu anazijua haki zake za msingi.
* Haijalishi ni watu wangapi watakuelewa katika kile unachokifanya / unachokisema au kile unachokiamini.
* Kuna nyakati lazima Farao akukimbize / akufuatie nyuma ndipo njia itakapopatikana.
* Kuna gharama za kulipa kufika daraja la kwanza (first-class / kiwango cha juu).
* Kuna wakati hakuna mtu wa kukubeba / kukusaidia, ni lazima ujitie nguvu mwenyewe. (David strengthened himself in the Lord).

3. Mtazamo (perception).

* Kile ambacho unakitazama / unakiona kwenye ubongo wako ndicho utakachokimiliki. Yesu hakumuona mariamu kama kahaba bali chombo chake. Akionacho Yesu lazima na sisi tukione.

Papaa Ze Blogger alimalizia kwa kusema hivi:
SIO KILA MKRISTO ANA VITA, BALI MWENYE KITU NDIE MWENYE VITA. I like this.


mdee junior na sam sasali papaa.



             










Born to praise team.















Mungu akubariki, Karibu NCHI YA AHADI.

Mawasiliano:


+255 659 700 002
+255 756 145 417

mdeejunior@gmail.com
mdee.junior (skype)
@mdee_junior (twitter)

Dream Big As You Grow Big.


Juu