Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

RIWAYA: JINAMIZI LA MABINTI

Unto Jesus every knee shall bow and tongue confess that He's Lord!

MTUNZI: ELIA MWAIPOPO

SEHEMU YA TATU (3)
*********************


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Siku ya saba akashushwa duniani akiwa ni binti tofauti na Yule wa zamani, ambapo
yasemekana uzuri wa macho yake angavu na kidevu kilichochongoka kwa ustadi mkubwa
vilizidi kuwa kivutio kikubwa kwa wasichana wenzake, hali kadhalika wanaume pia ambao
siku zote walikuwa wakitamani kuwa na binti huyo mrembo. Alikuwa ana kiuno cha
mduara kilichobinuka mithili ya kichuguu, ngozi yenye ulaini na unadhifu ulishikamana
sambamba na uasili wa nywele zake. Kwa vijana wengi safari hii alipewa jina la “ Maria
Cleopatra” (mwanamke anayeaminika kuwa ndiye mwanamke aliyewahi kuwa mzuri kuliko
wanawake wote ulimwenguni).
*********************
Kitu kikubwa na cha kushangaza ni kwamba Monica hakuonewa wivu na wasichana
wenzake tu bali hata wavulana pia. Kwa kawaida haikushangaza kusikia minong’ono
kuwa binti huyu alikuwa akijisikia au (kuwa na mapozi) kama wasemavyo vijana wa siku
hizi waliokulia mijini. Kuhusu mwendo wake mara nyingi ulizua taharuki kubwa na
mihemuko ya kihisia kwa vijana makapela na wazee hali iliyohamisha hisia zao huku wengi
wakihisi wapo dimbani wakisakata kabumbu na binti huyo. Utanashati sifa yake kuu kwani
tangu udogo wake hakuwahi kukutwa na matope wala kuvaa nguo kuu kuu, licha ya kuwa
na maisha ya kawaida katika familia ya Mzee Wazza Likuhusulo.
*************
ENDELEA………
Siku moja wakati wa sherehe za Krisimasi na Mwaka Mpya Monica alijumuika na vijana
wenzake katika sehemu moja ya starehe iliyoko karibu kabisa na upwa wa bahari ya hindi;
sehemu hiyo maarufu ndani na nje ya jiji la Dar es salaam ijulikanayo kama Coco beach
imejizolea jina kubwa sana hasa kwa wageni waingiao na kutoka nje ya jiji la Dar es salaam.
Umaarufu wa sehemu hiyo haukuja hivi hivi tu bali inasemekana ni kutokana na matukio ya
kihistoria ambayo yalikuwa yakizunguka na kutokea sehemu hiyo. Tangu ukoloni
inaaminika kuwa Watawala wa kikoloni hasa Wajerumani na Waingereza walipenda
kujumuika na familia zao katika sehemu hiyo ambapo ujio wao pahali hapo palichangia
kiasi kikubwa sana kuipa umaarufu upwa wa fukwe ya bahari hiyo kwa wakazi jirani na
maeneo hayo. Akiwa ni miongoni mwa wahudhuriaji na wageni wa eneo hilo monica
alifanikiwa kujipenyeza na kuwaambukiza nguvu za Madubwana hayotakribani mabinti
kama tisa wakiwamo Merina,sara,jackline,tinna,shamsa.
*****************************
wakia katika tafrija hiyo mabadiliko yalianza kuonekana taratibu kadri muda ulivyozidi.
Mvuto wa mabinti hao wadogo ambao ilikadiriwa kuwa na umri wa miaka kumi na tano
mpaka kumi na saba (15-17) hivi ulizidi kuzisumbua hisia za vijana wengi waliokuwapo
eneo la tukio. Wakati wa kipindi cha kuogelea kilipofika ndipo mboni za macho ya vijana
wengi waliokuwepo eneo la tukio hawakuamini kile walichokuwa wakikiona kwa mabinti
hao ambao hawakuwahi kuguswa na kiumbe chochote kile chenye jinsia ya kiume. Kifupi
mabinti hao warembo ambao walikuwa ni wabichi kama wasemavyo vijana wa ishio mjini
siku hizi, huku wengine wakiwa na mtanabaisho tofauti kwa mabinti hao na kuwaita
machenza; hakika ilikuwa ni siku huru kwa kila aliyekuwapo eneo la tukio ambapo
mawasiliano ya macho na ubongo wa kila aliyekuwapo eneo la tukio vilimvuta na
kuhitimisha matamanio ya kila aliyekuwapo ndani ya mioyo yao. Hakika ilikuwa ni siku ya
kustaajabisha na kuhuzunisha kwa vijana ambao walihisi wasingeweza kuwamiliki mabinti
hao.
*****************************
John, kijana msomi na mtanashati aliyekuwapo eneo la tukio wakati hayo yote yakiendelea
alijikuta anashindwa kuvumilia na kuamua kujisogeza taratibu kwa Monica ambaye wakati
huo alikuwa akiyanyonga maungo yake kama binadamu aliyekosa mfupa.

“Habari yako dada? Aliuliza John na kufungua pazia la mazungumzo kati yao “nzuri tu
mambo vipi kaka (Monica anajibu kwa sauti laini iliyomkosha John na kuzidi
kumuongezea hamu ya kusema zaidi na binti huyo) Naitwa John Peter, naishi Mbezi, vipi
naweza kupata mawasiliano yako dada? Naitwa Monica ninaishi Ubungo (river side)
mawasiliano ya nini kaka yangu?
**************
Mazungumzo yao yalisindikizwa kwa muziki wa taratibu uliosikika kando kando ya ufukwe
wa bahari hiyo, sasa ulikuwa ni muziki wa kimagharibi ambao ulikuwa ukipigwa na
hakuwa mwingine bali alikuwa ni mwanamuziki anayeaminika kuwa na sauti nyororo na
nzuri Shania Twain na kibao chake “Forever and for always” kilichokuwa na mistari
iliyowafanya vijana wengi kusogeleana karibu na kuanza kujizungusha taratibu wakiwa
wamekumbatiana. Kusikika kwa wimbo huu saa kuliamsha hisia za John na kumfanya
atumie vyema viungo vyake katika kumbembeleza mwanadada huyo, hapo taratibu
mikono ya John ilisogezwa naye kumshika Monica huku sauti ya John mwenyewe ikiwa ni
ya kubembeleza zaidi, aliivuta mikono ya Monica na kuisogeza taratibu kuzunguka kiuno
chake, sijui ni wimbo au sauti ya bembeleza iliyomsahaulisha Monica ugumu wa nafsi yake
katika kukubaliana na vijana wa kileo kwani taratibu alijikuta akifanya kile John
alichokitaka, wazo la mawasiliano ikiwa ndio kiini cha mazungumzo yao likatiwa kapuni
kwa sasa na kilichoibuka kati yao ikawa ni “Naomba tucheze basi” aliongea John na
kujibiwa kwa vitendo na kisura huyo aliyosheheni sifa zote za urembo, alimwangalia John
na kuachia tabasamu zito, safi na mwanana na kisha lips zake zikafungamana tena kama
aliyehesabiwa sekunde za kutabasamu, aliitoa mikono yake katika kiuono cha John na
kiuipeleka mabegani mwa kijana huyu, taratibu miguu yao ilianza kurandaranda katika
mchanga wa fukwe kuonesha nayo imeafikiana na maamuzi yao, kadiri wimbo ulivyosonga
mbele ndivyo umbali wa wawili hawa ulizidi kufifia na kisha kutoweka kabisa na kuwa ule
wa O distance kama wasemavyo wajuzi wa mambo haya. Wimbo huu ulizidi kuzibamba
nafsi zao….


In your arms I can still feel the way you
Want me when you hold me
I can still hear the words you whispered
When you told me
I can stay right here forever in your arms

And there ain't no way
I'm lettin' you go now
And there ain't no way
And there ain't not how
I'll never see that day


[Chorus]
Cause I'm keeping you
Forever and for always
We will be together all of our days
Want to wake up every
Morning to your sweet face always

Mmmm, baby
In your heart I can still hear
A beat for every time you kiss me
And when we're apart,
I know how much you miss me
I can feel your love for me in your heart

And there ain't no way
I'm lettin' you go now
And there ain't now way
And there ain't no how
I'll never see that day

[Chorus]
(I want to wake up every morning)
In your eyes (I can still see
The look of the one) I can still see
The look of the one who really loves me
(I can still feel the way that you want)
The one who wouldn't put anything
Else in the world above me
(I can still see love for me) I can
Still see love for me in your eyes
(I still see the love)

And there ain't no way
I'm lettin' you go now
And there ain't no way
And there ain't no how
I'll never see that day

[Chorus: x2]

I'm keeping you forever and for always
I'm in your arms

Kadiri maneno haya yalivyopenyeza na kupasua ngome za masikio yao ndivyo vijana hawa
walivyozidi kupata misisimko katika fikra zao na kufanya waliokumbatiana wazidi
kushikana vyema na waliokaa wakasimama wakianza kucheza nao kwa madaha wengine
wakitumia nafasi hizi kuomba mahusiano ya kudumu huku walio tayari katika hili
wakiweka ahadi za uchumba………
 


INAENDELEA.......

Juu