Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

KIOO CHA BLOG: SAFARI YA HANA KUELEKEA MAJIBU.

   Nakusalimu kwa Jina la Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Amina.

   Katika kioo cha blog hii, leo tunatazama siri ya kuelekea majibu yadumuyo. Mtumishi wa Mungu Hana katika kitabu cha 1Sam ndiye KIOO chetu cha leo. Kumbuka kuwa Mungu alimfunga tumbo asizae, lakini ilikuwa ni kwa ajili ya Utukufu wake mwenyewe (MUNGU), hatimaye Bwana akamuona na kumpa uzao baada ya kumlilia sana! Hana alienda mbali zaidi ya ukawaida wa Wakristo wengi wa sasa (beyond normality).

   Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi sana ni kwa nini tunaomba sana au tunaombewa sana lakini hatuoni matokea halisi na mabadiliko katika maisha yetu? na yakiwepo matokea kwa nini yanakuwa ni ya muda mfupi tu? Tatizo liko wapi? Je! mimi ninayeomba/kuombewa ndo nina tatizo? na je tatizo liko wapi? je! nalitambua tatizo? Majibu ya maswali haya ndio mpenyo na ufunguo wa majibu ya maombi tuombayo/uombayo.

   Wakristo wengi kama sio wote tumekuwa na tabia sugu ya uvivu na kuridhika (complacent) kwa matokeo hafifu tuyaonayo. Hatupendi kuomba, tunasubiria kuombewa; na tukiomba twaomba emotionally/kihisia sio kwa target/kulenga, hii inatufanya tuwe tegemezi.

   Hebu kwa pamoja kupitia KIOO cha blog tumtazame Hana, yumkini anayo majibu.

1Samuel 1:1-20.
   Wakristo wengi tumekuwa na tabia ya kutegemea maombi ya kuombewa na watumishi wa Mungu. Na hii ni kwa sababu tumeishia tu kutambua hitaji tulilo nalo  na sio uhitaji wa hitaji (requirements of the need).
Mfano; unahitaji Mungu akupe mume/mke, na hilo ndio hitaji lako; lakini ufanye nini ili upate hitaji lako kwa wakati na majira sahihi kutoka kwa Bwana, huo ndio uhitaji wa hitaji lako. Hapa ndipo kuna tatizo, kutambua uhitaji wa hitaji na mwisho wa siku tunaanza kupeperushwa na upepo wa huduma za maombezi(sipingani na huduma za maombezi) la hasha! Nataka Mkristo afike mahali aweze kusimama yeye kama yeye na Mungu wake kwa sababu watumishi wanaotuombea wana nafasi yao, Mungu naye ana nafasi yake na sisi tuna nafasi zetu ili Mungu atende(we must play our part). Tusiwabebeshe watumishi wa Mungu nafasi zetu/wajibu wetu kwa Mungu wetu, nasi tutapona.
Nataka nikuambie, usipotambua nafasi yako, na uhitaji wa hitaji lako utawekewa mikono, miguu na mwisho wa siku utafanyiwa maombi yanayoambatana na kupigwa makofi lakini hutaona badiliko lolote kwa maisha yako. Tatizo ulilo nalo lisikufanye uwe yatima wakati unaye Baba anayekujali, badilika sasa na badilisha mfumo wako wa maombi.

Mstari wa 4-5
   Eli anaonesha kumpenda sana Hana hata kumpa sehemu mara mbili kwa ajili ya dhabihu. Eli hakutambua uzito/uhitaji wa hitaji la Hana mkewe.

Mstari wa 8.  Tunaona Eli akimfariji Hana kwa maneno mazuri sana akisema; Je! mimi si bora kwako kuliko watoto kumi? Ni kweli ametumia lugha nzuri inayoonesha kujali/kupenda na kuthamini akimaanisha kuwa nakupenda hata kama huna mtoto, pamoja na lugha zote na matendo yote yaliyoonesha Eli kumpenda Hana vile alivyo bado haikuweza kugusa tatizo la Hana. Ukweli ulibaki pale pale kuwa Hana bado hana uwezo wa kuzaa.

   Mwisho wa siku Hana anafunguka, moyo wake ulijaa huzuni, macho yake yalijaa machozi hata asiweze kula, alikuwa na uchungu rohoni mwake. Faraja kutoka kwa Eli, kuhani haikumsaidia kitu, ilikuwa ni faraja ya muda tena inawezekana Eli, kuhani alithubutu hata kumwekea mikono na kuomba pamoja naye lakini bado jibu halikutokea/lilifichwa.
Hatimaye Hana akatambua kuwa hakuna majibu kwa mwanadamu wala kwa mumewe, wala kwa fedha, mali na utajiri wao.

   Hana hakutaka tena kulialia mbele za watu wala hakutaka faraja ya mwanadamu, ndipo alipoamua kuinuka akamwacha Eli kuhani na kuingia hekaluni peke yake mahali ambapo mchungaji hakuwepo wala mtume, wala nabii, wala kwaya, wala praise and worship team haikuwepo bali alikutana na UWEPO wa mzee wa siku Mungu Jehovah ndilo Jina lake. Mstari wa 9-10. Biblia inasema kuwa Hana alimuomba Bwana huku akilia sana.
Hebu tujifunze kumtafuta Mungu na uwepo wake mana ndiko kuliko na majibu yetu. Hana akaeleza uhitaji wake mbele za BWANA.

   Inawezekana unapita katika nyakati ambazo kila akutazamaye anakuona duni, si kitu, haufai, unadharauliwa; Lakini usife moyo huo sio mwisho wa maisha yako. Tambua uhitaji wa hitaji lako, ingia nyuani mwa Bwana, mimina roho yako mbele zake, Hakika utatoka hapo ulipo na hutakuwa kama ulivyo leo.Kataa upepo wa kukimbilia maombezi kila mahali unaposikia kuna maombezi, jifunze kufanya sehemu yako kwanza. Hana akamjibu Eli, kuhani ''Usimdhanie mjakazi wako kuwa ni mwanamke asiyefaa kittu'' haya ni maneno ya kuchoshwa na hali aliyokuwa anapitia.
 
   Baada ya maombi mazito ya ufunuo, Hana alitoka hekaluni (uweponi mwa Mungu) akiwa na furaha tele na amani wala uso wake haukukunjamana tena maana aliingia hekaluni akiwa na roho ya uchungu huku akilia sana na uso wake ulikunjamana sana tena hakuweza kula chakula, lakini hali yake ilibadilika baada ya kukutana na Rehema za Bwana hekaluni. Furaha ikarejea na amani akaweza kula chakula maana kabla ya hapo chakula kilikuwa hakishuki! Mstari wa 18.
Uwepo wa Mungu hubadilisha maisha ya mtu rohoni na mwilini na kumfanya kuwa mtu mpya tena humuondolea aibu.
   Hitaji la hana lilikuwa ni kupata mtoto tena mtoto mume; na uhitaji wa hitaji lake ulikuwa ni kutafuta na kukaa uweponi mwa BWANA na kumimina roho yake/hitaji lake , kuwasilisha haja yake kwa Bwana na sio kwa wanadamu ambao leo wapo kesho hawapo, leo wanakuchekea kesho wanakung'ong'a na kukusemea mabaya.


HITIMISHO:
Majibu ya Hana yalitokana na yeye kutambua nafasi yake na kuingia katika utendaji kiuhalisia.

Je! tatizo ulilo nalo limekufanya uonekane duni, usiyefaa, si kitu si lolote, hata jamii inayokuzunguka imekukatia tamaa na kukudharau; au ndoa ya iko hatarini (ICU) kwa sababu huzai hata mume amekuwa na nyumba ndogo.

TAMBUA NAFASI YAKO, SIMAMA NA MUNGU, kama alivyomtokea Hana atakutokea na wewe leo kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth Mwana wa Mungu Aliye Hai.


   Bwana Yesu, kwa utukufu wa jina lako takatifu na kwa Damu yako ya thamani; nakusihi/naomba roho ya ufufuo kwa ndugu yangu huyu ambaye anafuatilia KIOO cha blog hii, kutana na uhitaji wa hitaji lake kwa jina lako Yesu. Kila mara anyoshapo mikono yake kuelekea hekaluni mwako/madhabahuni pako naomba umsikie na kumtendea muujiza zaidi ya vile ulivyotenda kwa mtumishi wako shujaa HANA. Na kila aitiapo msaada wako Eeh BWANA ukashuke na kumsaidia, zaidi sana macho ya moyo wake yatiwe nuru yapate kuona maajabu yatokayo katika sheria yako ambayo ni Neno lako, pia ukampe neema ya kutambua uhitaji wa hitaji lake pale apitiapo nyakati ngumu au mazingira yeyote yale na akawe mwanafunzi mwaminifu katika hali zote anazozipitia au atakazozipitia katika maisha yake. Mpe neema ya kipekee kuvuka ng'ambo ya bahari/ng'ambo ya ufahamu alio nao sasa apate kukujua zaidi na kukufuata wewe peke yako. Mpe kuitambua nafasi yake na kile anapaswa kuwajibika kwacho.
   Kwa Jina La Yesu Kristo, nimeomba na kuamini kuwa ndugu yangu huyu amepokea na ya kuwa hakika hutamwacha hata nukta moja. AMINA!



















Kwa Msaada zaidi au Maoni wasiliana:

+255659 700 002
+255756145 417
mdeejunior@gmail.com
@mdee_junior (twitter)
mdee.junior (skype)

DREAM BIG AS YOU GROW BIG!





 






Juu