Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

CAPACITY BUILDING CLASS: NIDHAMU KATIKA MUDA Na MC. Harris Kapiga NDANI YA NCHI YA AHADI..

  
Harris Kapiga ni mtu ambaye kwa muda mfupi nilioweza kumsikiliza nimeweza kujifunza vitu vingi sana katika maisha yangu, ushuhuda wa maisha yake unaweza kubadilisha maisha ya mtu yeyote yule ambaye amefika mahali pa kujiona kuwa si chochote silolote anasubiria kufa tu biashara iishe. Natamani kama wewe ni mmoja wapo miongoni mwa watu waliofikia hatua hii, fanya maamuzi ya kuonana na Mc. Harris Kapiga. Mwanzoni mwa blog hii kuna tangazo linasema KARIBU NCHI YA AHADI MINISTRY, Tumia namba ya simu iliyopo hapo au mwishoni somo hili utaona mawasiliano hapo pia unaweza kutumia.


   Baada ya utangulizi huo mfupi naomba twende moja kwa moja kwenye somo la leo linalosema NIDHAMU YA MUDA sanjari na DONDOO KUMI BINGWA KATIKA KUKUWEZESHA KUTUMIA MUDA WAKO, aliyefundisha somo hili ni MC. HARRIS KAPIGA mwenyewe!

Harris alianza na swali kwa umati wa watu waliokuwa wamehudhuria!

MUDA NI NINI? Kila mtu alijibu vile alivyoweza kwa ufahamu na mtazamowake; mwishoni Harris akaja na jibu sahihi kabisa lililomfaa kila aliyehudhuria na ninaamini hata wewe litakufaa sana na utakubaliana naye.

Muda ni kipindi ambacho vitu hutokea _ Time Is a point or a period at which things occurs. Aliendelea kufafanua kuwa kuna aina mbili za muda.

KUNA AINA MBILI ZA MUDA.

1. Muda wa saa (clock time) 
Yaani muda wa saa tulizo nazo kila siku; mfano. katika dakika moja kuna sekunde 60, siku moja ina masaa 24, mwaka una siku 365. Muda wa saa uko fixed maana yake ni kwamba ukipita umepita huwezi kuubadilisha / kuurudisha nyuma. Kwa maana hiyo basi Muda wa kwenye saa hauhusiki na maisha yetu kwa uko fixed.

2. Muda halisi (Real time).
Muda halisi ndio muda wenyewe hasa unaohusika na maisha yetu na tunapaswa kupeleka macho yetu huko. Mfano. unaweza ukakaa mahali mwezi 1. ukadhani umekaa miaka 10 au ukakaa mwaka 1. ukadhani siku moja kulingana na mazingira halisi ya hapo mahali.
Muda halisi ni muda ambao uko kwenye akili, muda halisi unautengeneza wewe. Na kitu halisi unachokitengeneza wewe unaweza kukimiliki. Ukiutengeneza muda wako una uwezo wa kuumiliki.

NJIA TATU ZA KUTUMIA MUDA WAKO.
Kila mtu anaweza kuangukia katika moja ya njia hizi.

1. Kufikiri 2. Mazungumzo / kupiga stori. 
Mfano; ukiwa peke yako na hufanyi kitu chochote lazima kuna vitu vitakuwa vinaendelea ndani yako, unafikiri / unasemezana na nafsi yako; hapo utakuwa unatumia muda.

3. Vitendo / kitendo.
Namna ya kutumia muda imekuwa tatizo sana, tunatumia vibaya rasilimali ya muda. Ni bora kutengeneza muda wako kwa sababu muda wa saa huwezi kuukimbiza, ukipita umepita (clock time). Swali la kujiuliza; je! tangu umeamka umefanya nini au sasa hivi unaposoma ujumbe huu unafikiria nini?
Mafanikio yako katika kitu chochote yanategemea unatumiaje muda wako katika mambo hayo matatu. Zingatia; chochote unachokifanya au unachokitenda lazima kikunufaishe wewe na huko ndiko kutumia muda kwa faida.
Katika kufikiri kuna vitu vizuri vinapita kwenye akili, hivyo basi ni lazima unapokuwa mahali popote hakikisha unakuwa na kijitabu ili uweze kuandika kila wazo linalokujia akilini. Tumia muda wako mwingi kwa kufikiri _ positively. Usipoteze muda wako kwa mazungumzo ambayo hayakuletei faida kwa sababu yatakuwa yanakupotezea muda bila mafanikio.

DONDOO KUMI (10) KATIKA KUKUWEZESHA KUTUMIA MUDA WAKO.

Lazima utambue thamani ya muda ambao unaishi duniani. Kama hautafika mahali ukawa mjeuri hakika utapoteza muda wako. Ukiwa na nidhamu ya muda watu wengi watakuona wewe ni mjeuri kwa sababu utakuwa kinyume na ratiba zao. Mfano ratiba yako inaonyesha muda fulani utakuwa mahali fulani ukifanya jambo fulani, halafu muda huo mtu anakupigia simu eti muende kwenye harusi, sasa ukimuambia sitaweza kwenda kwa sababu nina kazi ni rahisi sana akakuona wewe ni mjeuri tena unaringa.

1. Hakikisha unaandika Ratiba ya Matukio / Vitu / mambo unayoenda kufanya.
Pangia vitu vyako ratiba ya siku. Tanguliza kile ambacho kinakuletea faida. Kabla hujaamka lazima ujue utafanya nini. Fahamu ratiba yako ya siku utafanya nini au kama huwezi ya siku panga ya wiki.

2. Shughuli yeyote / mazungumzo ya maana katika kukuletea mafanikio lazima uyapangie muda, utaanza saa ngapi na utamaliza saa ngapi.
Kitu chochote ambacho ni cha maana katika maisha yako lazima ukipangie muda.

3. Panga kutumia angalau asilimia hamsini 50% ya muda wako katika mawazo au shughuli zenye matokeo ya kukunufaisha wewe. Mfano; naweza kutumia muda wa kufikiria jinsi gani naweza kuiboresha kazi / shughuli ninayoifanya ili iweze kuwa na utofauti na za wengine. Hii itakusaidia kuboresha kile ulicho nacho na mafanikio yake huwa makubwa sana. Lazima utoboze. (Creativity)

4. Angalau tenga dakika 30. za kupanga ratiba yako ya siku.
Ni marufuku kuanza siku yako kama hujaandaa ratiba ya siku inayofuata.

5. Usione aibu kumwambia mtu, samahani sitaweza kuja au usije nina kazi au usinisumbue nina kazi.
Ukiishi kwa kuwafurahisha watu, mwisho wa siku utaumia (itakula kwako). Na huu sio ujeuri m'baya au kiburi au tabia mbaya, hapana ni NIDHAMU. Nidhamu ya muda ni kanuni ya maisha na kufanikiwa (hapa nimeongezea)

6. Jizoeze kutokujibu sms au kupokea simu kwa sababu tu unataka kupokea au kujibu.
Panga muda maalum wa kujibu sms au kupokea simu.

7. Wakati mwingine unaweza ku-block social networks mfano facebook, twitter n.k. kama unaweza, lengo ni kutumia muda kwa manufaa. Hebu jaribu kufikiria miaka kumi nyuma, halafu angalia umefanya nini katika hiyo miaka kumi? halafu fikiria miaka kumi ijayo utakuwa umefanya nini?


mdee junior (mwanaharakati).
   Ki-ukweli baada ya Harris Kapiga kuuliza swali hili, nilitulia kama dakika moja hivi nikafikiria miaka kumi iliyopita; huwezi amini ilinilazimu nijikaze kuzuia machozi yasitoke kwa sababu nilijiona nimepoteza muda mwingi sana halafu hakuna cha maana nilichokifanya ambacho naweza kukionyesha kwa watu.
NB. Siku 21 zinatosha kabisa kubadilisha tabia.

8. Kabla hujapiga simu yeyote jiulize:
a> unataka kupata nini katika simu hiyo, kama ina mantiki na inakunufaisha, piga. Ukitumia muda vizuri kutakuletea maendeleo. Piga simu zenye tija au sms zenye tija.

9. Tenga muda wa kuchat na kupiga simu unazotaka kupiga.
Hakikisha huo muda ulioupanga ukiisha hama hapo ondoka anza kitu kingine kulingana na jinsi ulivyopanga.

10. Wakati mwingine huwezi kumaliza kila kitu lakini hakikisha basi mawazo / mazungumzo yako yanakunufaisha / yanakufaidisha asilimia themanini 80%.

Harris Kapiga ni Mc. na ni Mchungaji kiongozi katika huduma ya NCHI YA AHADI.; pia ni mtangazaji wa kipindi cha Gospel Tracks na Temino, Clouds Fm Radio.

Kama umebarikiwa au unataka kufika nchi ya ahadi unakaribishwa na semina hizi zinafanyika kila siku ya jumapili kuanzia saa tisa alasiri.
Mungu akubariki kwa kushiriki pamoja nami baraka hizi. Ukifanyia kazi hiki ulichojifunza, hakika UTATOBOZA TU! FIKA NCHI YA AHADI UPATE MENGI ZAIDI.

KUMBUKA: 
Kama ambavyo Blog hii imekuwa ikikuletea mafundisho yenye kubadilisha ufahamu/akili na maisha kwa ujumla; Unaweza kui-support Blog hii kwa kununua mafuta halisi ya alizeti yenyo ubora wa juu, Lengo ni kufanikisha Blog hii Iendelee kukuletea mafundisho mazuri kutoka kwa watu maarufu na waliofanikiwa ambao nimekuwa nao bega kwa bega ili kuhakikisha msomaji wangu anapata kitu kitakachoweza kumtoa hatua moja kwenda hatua nyingine!
   Ili kujipatia Mafuta haya waweza kuwasiliana nasi kwa  0659 700 002 na Mungu atakubariki.
Asanteni sana wadau wangu! 


HJ



Mawasiliano:

+255 659 700 002
+255 756 145 417

mdeejunior@gmail.com
mdee.junior (skype)
@mdee_junior (twitter)

Dream Big As You Grow Big.




KUKUA KIROHO (SPIRITUAL LEVELS) NA SAM SASALI a.k.a Papaa NDANI YA NCHI YA AHADI JUMAPILI YA LEO.

Ze blogger Sam Sasali, Papaa leo alishusha nondo za ukweli kama sio misumari ndani ya huduma ya Nchi Ya Ahadi iliyo chini ya mchungaji kiongozi Harris Kapiga, Sinza Kamanyola; Dsm.

Andiko lililokuwa limebeba ujumbe mzima lilitoka kwenye kitabu cha Wagalatia 4:1...
''Mrithi awapo mtoto hana tofauti na mtumwa ingawa ni bwana wa wote''. Atakuwa chini ya uangalizi mpaka wakati ulioamriwa na baba (Mungu).
* Ishu hapa sio kwamba urithi haupo la hasha ila ishu ni kwamba Mrithi ni mtoto na mrithi akiwa mtoto ni sawa sawa na mtumwa.
* Tatizo sio kwamba Mungu hajatupa ahadi bali tatizo ni level / viwango katika kuiendea ahadi.
* Kila mtu anapewa kulingana na level aliyo nayo.

1Sam 17:16-17.  Kuomba vibaya sio yale maneno unayoongea mbele za Mungu bali NIA uliyo nayo juu ya kile unachoomba kwa Mungu.
* Unapokaa vizuri na Mungu hata level yako ya kukua inaongezeka.
* Hatumjui Kristo kwa kuimba mapambio.
* Shetani hana haja/agenda na mimi au wewe bali ana agenda na kile ulicho nacho / kile kilicho nyuma yako ambacho kinaweza kukupeleka level nyingine.
* Shetani hakuwa na agenda na Adamu au Eva bali kile walichokuwa nacho; alilenga kile walichokibeba. Adamu alipewa agizo asile tunda hivyo agenda ya shetani ilikuwa ni lile agizo alililopewa Adamu na Mungu.
* Yesu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea, kilichopotea hapa sio mtu bali ushirika kati ya mtu na Mungu (fellowship).

MAENEO YA KUONGEZA LEVEL / VIWANGO.

Mfalme yule alitoa talanta kwa kila mjoli wake kulingana na level / uwezo wa kila mtu.
Ugomvi wa Mungu na mwanadamu ni UTII / OBEDIENCE.

1. Kulifahamu / kulisikia na kulijua Neno la Mungu.
Mungu huzungumza kupitia Neno lake.
Level au uwezo ulio nao lazima utofautiane na yule anayeokoka leo. Kila mtu anakua (growth) kutokana na level aliyo nayo.

* Yesu anapotoa mwaliko ''njooni kwangu nyote wenye kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha'' Swali linakuja, je! nini kinafuata baada ya kupumzika?
Hahahhaaa ts funny, Baada ya kupumzika unakuwa umepata nguvu mpya za kukuwezesha kubeba mizigo yako uliyo nayo na kuendelea na safari yako kwani utakuwa na nguvu za kubeba hiyo mizigo/ jaribu ulilo nalo mara baada ya kupumzishwa na kujifunza miguuni kwa Yesu jinsi ya kuendelea na safari. Maana asema hivi; mjifunze kwangu, hivyo kuna shule ya kujifunza hapo kwa sababu Yesu hajasema njooni mniachie mizigo yenu bali njooni niwapumzishe then mwendelee na safari yenu.
* Ukristo ni mchakato endelevu. / Continuous Process. Lazima tukue katika kulisoma Neno la Mungu.

2. Maombi (sio maombezi).
* Watu wengi wanaopenda maombezi hawana Neno ndani yao. Mtu mwenye Neno / aliyejaa Neno ana maneno mengi ya kumwambia Mungu kwa sababu anazijua haki zake za msingi.
* Haijalishi ni watu wangapi watakuelewa katika kile unachokifanya / unachokisema au kile unachokiamini.
* Kuna nyakati lazima Farao akukimbize / akufuatie nyuma ndipo njia itakapopatikana.
* Kuna gharama za kulipa kufika daraja la kwanza (first-class / kiwango cha juu).
* Kuna wakati hakuna mtu wa kukubeba / kukusaidia, ni lazima ujitie nguvu mwenyewe. (David strengthened himself in the Lord).

3. Mtazamo (perception).

* Kile ambacho unakitazama / unakiona kwenye ubongo wako ndicho utakachokimiliki. Yesu hakumuona mariamu kama kahaba bali chombo chake. Akionacho Yesu lazima na sisi tukione.

Papaa Ze Blogger alimalizia kwa kusema hivi:
SIO KILA MKRISTO ANA VITA, BALI MWENYE KITU NDIE MWENYE VITA. I like this.


mdee junior na sam sasali papaa.



             










Born to praise team.















Mungu akubariki, Karibu NCHI YA AHADI.

Mawasiliano:


+255 659 700 002
+255 756 145 417

mdeejunior@gmail.com
mdee.junior (skype)
@mdee_junior (twitter)

Dream Big As You Grow Big.

MSAMAHA / FORGIVENESS

   Msamaha ni nini, kwa nini tusamehe, nini matokeo ya kutokusamehe? Fuatana nami katika series hii ya fundisho la msingi.

   Mdee Junior, mtumwa wa Yesu Kristo, ndugu yake msomaji wa blog hii, kwa hao walioitwa, waliopendwa katika Mungu Baba, na kuhifadhiwa kwa ajili ya Yesu Kristo, wapate neema ya kusamehe kama vile Kristo Yesu alivyowasamehe. Mwongezewe rehema na amani na upendano ndio tunda la roho ya msamaha. AMINA.

   Msamaha ni: Kufuta deni, kuhurumia, kupatanisha, kuleta / kurudisha mahusiano yaliyovunjika / potea. Ni tendo la upendo, na upendo hauhesabu mabaya.

Msamaha ni kanuni ya MAISHA, Yatupasa kusamehe kwa sababu hatukuitwa ili kubeba hali ya kutokusamehe.

* Iko nguvu inayohuisha ndani ya msamaha ndio maana baada ya kupokea msamaha wa Yesu Kristo unajisikia kuwa mtu mpya / unahuishwa upya.
* Tunapovunja kanuni ya msamaha, tunavunja kanuni ya maisha. Kukataa kuomba msamaha / kusamehe wengine ni KIBURI- maana Mungu alitusamehe.
Samahani ni neno dogo lakini linaweza kusababisha maelfu kuangamia / kuponywa, kanisa kujengwa / kubomoka; laweza kuleta umoja imara / kuvunja umoja, pia laweza kurudisha upendo au kuleta chuki na visasi.
Neno  nimekusamehe linarudisha mahusiano, linaponya na limeponya wengi. Kutokusamehe kunaonyesha uchanga wa kiroho. Pia kunafunua au kuonyesha mahusiano kati ya mtu binafsi na Mungu jinsi yalivyo.
* Kusamehe ni kufuta kila kitu na kuanza upya, na hii inaonyesha mahusiano yaliyo imara na thabiti kati ya mtu binafsi na Mungu na huu ndio UKOMAVU WA KIROHO.

YESU AKASEMA IMEKWISHA.

Yesu kusema imekwisha, maana yake ni kwamba alitusamehe kwa kutuhurumia na ndio maana;
* Tunasimama siku zote kwa sababu ya msamaha wa Bwana Yesu.  Waebrania 12:2b
   'Ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu'...
Watu wengi wameshindwa kuomba msamaha kwa sababu wanahisi wataradhauliwa na kuonekana duni, lakini kumbuka kuwa Yesu hakuwa na mtazamo hasi kama huo ndio maana Biblia inasema kwamba ALIIDHARAU AIBU. Hata kama utadharaulika, ni lazima usamehe maana hii ndio kanuni ya maisha ya Ki-Mungu.
* Yesu ametuachilia na kutuweka huru.

KUTOKUSAMEHE KUMESABABISHA MAJERAHA MENGI - HURTINGS.

Mathayo 18:21-35; Wakolosai 3:14
   Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? hata mara saba? Yesu akamwambia, sikuambii hata mara saba bali hata saba mara sabini.

   Ndugu yangu hapa ndipo kazi ilipo. Kutokusamehe kumesababisha majeraha ya nafsi na uchungu mwingi ndani ya mioyo ya watu wengi. Biblia pia inasema, 'hampati kwa sababu hamuombi' sio kwamba hatuombi kweli bali kwa sababu mioyo imejaa uchungu hivyo hata tuombapo kinachotutoka ni UCHUNGU sio maombi.
   Ili uweze kupona inakubidi ufungue mlango katika moyo wako na kumtoa moyoni yule aliyekuumiza na kukusababishia makovu / maumivu / majeraha; umsamehe na kumwachilia kabisa. Msamaha huleta uponyaji, maisha ya msamaha ni ya kila siku; huwezi kuwa na mahusiano mazuri usiposamehe.
Unapotaka kusamehe usiangalie tatizo linalohusika hata kama wewe ndie una haki bali mtazame Yesu Kristo Msalabani. Yesu hakuwa na hatia yeyote iliyomfanya ateswe na kudharauliwa hata kutemewa mate lakini katikati ya maumivu hayo makali alisema; BABA WASAMEHE kwa maana hawajui walitendalo.

* Mstari wa 21. Hapa Yesu alimaanisha hivi; '' Petro, kumbuka nimekusamehe mara ngapi? hivyo endelea kusamehe sio mara saba tu bali saba mara sabini.
* Biblia inasisitiza juu ya msamaha kwa sababu ndiko kuna UZIMA. Uzima ulitolewa kwa njia ya msamaha - IMEKWISHA.
* Kusamehe sio kujaribu kusahau maumivu / kusukuma hisia chini au kudharau maumivu. Sema kweli / kuwa wazi na mwambie Mungu-Bwana nimeumia.
* Hakuna wakati maalumu wa kusamehe, kusamehe ni wakati wote (24hr) tunawasamehe watu wanapotukosea pia usimwendee mtu huku ukimwonyesha makosa.

   Mstari wa 27. 'Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni'. Kumbe msamaha ni tendo la kuhurumia na lina nguvu ya kipekee katika ulimwengu wa roho maana sisi ni roho.
Usipomsamehe mwenzako, unakuwa umemuweka kifungoni kwenye ulimwengu wa roho na wewe pia maana unajifungia mlango wa kutokusamehewa na kufanikiwa.

   Mstari wa 28-34; Inatuonyesha madhara ya kutokusamehe, kama Mungu kupitia Yesu Kristo aliweza kutusamehe, je! mimi ni nani hata nishindwe kusamehe? Mungu naomba nipe roho ya kusamehe na moyo wa kuachilia.
   Mstari wa 35; Msamaha ni lazima utoke moyoni maana kuna tofauti ya kusamehe na kugandamiza hisia (kubali yaishe).
   Mathayo 6:14-15; Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
Matokeo mengine ya kutokusamehe ni kwamba:
1. hutasamehewa
2. Unabeba na kutembea na watu moyoni
3. unakuwa na uchungu juu ya watu waliokuumiza; haya yote yanavunja umoja wa mtu na mtu hata na kwa kanisa pia.
4. unafungua mlango wa wewe kushambuliwa katika nafsi yako na shetani, maana shetani anaifahamu kanuni ya msamaha.
5. Utakuwa unaishi maisha ya mambo / vitu vilivyopita - Isaya 43:18-19. Na matokeo yake ni uchungu-kukandamizwa-roho ya uasi-kupagawa hasira.
Yesu alijua kanuni ya msamaha, naye alikuja ili kutufundisha na kutuingiza katika darasa / shule ya msamaha.

AINA YA MSAMAHA.

1> Kujisamehe wewe mwenyewe; ni ile hali ya kukubali na kuamini kuwa Mungu amekusamehe baada ya kuomba msamaha na kutubu mbele zake. Usikumbuke yaliyopita maana Mungu ana mpango mpya.

2> Samehe wengine; mfano. wazazi wengi wameumiza watoto wao kwa sababu nao waliumizwa. Hivyo samehe wazazi wako, viongozi, jamaa na marafiki zako hata kama wapo mbali nawe.

3> Msamehe Mungu. Kuna wakati Mungu anapofanya kazi yake ndani yako unakuwa unahisi maumivu na kwamba  amekuacha au hakuoni hali ambayo inaweza kukuletea maumivu makali na kumchukia Mungu na kukufanya uwe mtu wa kumlalamikia Mungu kitu ambacho ni kosa. Hivyo msamehe Mungu kwa kumuacha na kumruhusu amalize kazi aliyoianza ndani yako.

4> Samehe tetesi zote. Yale mambo yote yanayosemwa kinyume juu yako, samehe songa mbele huku ukimtazama yeye aliyekuita maana ni mwaminifu hatakuacha.

UNAWEZAJE KUSAMEHE.

a/
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu hutupa upendo wa kuwapenda adui na neema ya kuwaachilia.

b/ Uwe tayari kusamehe. Peleka moyo wako / hisia zako kwa Mungu naye atakupa neema ya kusamehe. Hisi zako ndio alama (indicator) pekee inayokuonyesha / ashiria kama umesamehe au la!

c/ Jenga uhusiano na adui yako; kula naye, fanya kazi pamoja naye, shirikiana naye.
Msamaha huleta mawasiliano.

HITIMISHO:
UKIJAA UCHUNGU NA MASHUTUMU; UTAKACHOKITOA NI UCHUNGU NA MASHUTUMU.

Mungu wangu na akubariki sana kwa kufuatilia somo hili la msamaha; naamini limekutoa sehemu moja na kukupeleka hatua nyingine mpya katika ukuaji wako wa kiroho na kujenga mahusiano imara kati yako na Mungu na wale wote wanaokuzunguka.
Nimejaribu kukueleza kwa kifupi tu kuhusu msamaha, lakini kama utahitaji ufafanuzi zaidi au kuonana nami ana kwa ana, na kama unahitaji msaada zaidi kuhusiana na kanuni nzima ya msamaha, kama unahitaji maombi; usisite napatikana na nipo tayari kukuhudumia. Wasiliana nami kwa moja ya mawasiliano hapo chini. Pia itakuwa njema kama utaacha comment zako hapo chini. Elezi vile ambavyo Bwana amekufungua kupitia somo hili. AMINA.

Bonyeza hapa kusoma makala zingine za kiuchumi.


MAWASILIANO:

Mobile: +255 653 100 100
Email: mdeejunior@gmail.com
Instagram: wasemeetz

Holding on to the hurt doesn't make it better. If you'll let it go and move forward, God will make it up to you.

GOD BLESS YOU

Mdee F. Junior




WATU WENGI WAZIDI KUFUNGUKA KUPITIA SEMINA ZINAZOFANYIKA KATIKA HUDUMA YA NCHI YA AHADI CHINI YA MCH. HARRIS KAPIGA! MADA KUU_''SELF DISCIPLINE''

   
Baada ya kutoka kwenye engagement siku ya jana, blog hii ilielekea moja kwa moja kwenye huduma ya Nchi Ya Ahadi inayoongozwa na Mch. Mpakwa Mafuta, HARRIS KAPIGA. Ambapo seminar isiyokuwa ya kawaida (yenye kubadilisha maisha na mtazamo wa mtu binafsi, personal life changing) ilifanyika kanisani hapo.

   Fundisho kuu lilikuwa ni ''NIDHAMU BINAFSI'' a.k.a SELF DISCIPLINE.
Wazungumzaji wa semina hii walikuwa ni; JAMES MWANG'AMBA (THE CHAMPION), TIMOTHY KYARA na ABELLA BATEYUNGA (MZALENDO).


HIKI NDICHO ALICHOZUNGUMZA JAMES MWANG'AMBA.



James Mwang'amba kabla ya chochote alianza kwa kusema hivi; ''USIPOKATA TAMAA UTASHINDA, USHINDI NI LAZIMA'' Baada ya kusema hivyo ndipo akaingia kwenye mada yenyewe! Twende pamoja naye sasa.





NIDHAMU:

Nidhamu ni uwezo wa kufanya mambo / vitu fulani pasipo kufuata hisia (kinyume na ulivyozoea). Baada ya kutoa tafsiri hiyo fupi iliyobeba shehena ya maarifa na uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu binafsi, James alizungumzia na kufafanua maeneo nane (8) ambayo yanahitaji nadhamu kali.

UNATAKIWA UWE NA NIDHAMU KALI KATIKA MAENEO NANE (8).

1. Eneo la kujiwekea malengo binafsi kila mwaka.

* Kujiwekea fursa/possibilities; mfano. mwaka huu nitafanya a, b, c... ukiendelea zaidi utatoka kwenye mwaka itakuwa malengo ya mwezi hatimaye kila siku.
* Mtu mwenye malengo anajua kule anakoenda, mtu asiye na malengo hawezi kwenda na hajui anakokwenda.
* Malengo yanakupa uwezo wa kudhibiti mabadiliko ya maisha katika dunia.
* Malengo yatakupa FOCUS.
* Siri moja ya mafanikio duniani ni kuwa na FOCUS.
* Malengo yatakufanya uwe namba moja (1), Mafanikio yanakuja kwa kufanya yale uliyojiwekea kuyafanya.

2. Nidhamu ya kufikiri vizuri / clear thinking.

* Ni uwezo wa kufikiri vizuri bila bughudha.
Hapa ananukuu msemo mmoja usemao; Those who cannot go within cannot go without.
* Mali ni uwezo wa mtu kufikiri vizuri / uwezo wa kutumia akili vizuri/zaidi.
Nukuu chanya: 'TATIZO SIO UDONGO TULIO NAO BALI UBONGO TULIO NAO'
* Njia rahisi ya kufikiria vizuri ni kuuzoeza ubongo kufikiri.

3. Nidhamu ya kutunza muda / time management.

- Tatizo tulilo nalo ni kutokutunza muda.
* Maisha ya mtu yeyote yanawakilishwa na kitu kidogo kinachoitwa muda, ukipoteza muda unapoteza maisha yako.
* Kimsingi maisha yako ni muda wako, na muda wako ni maisha yako. Jaribu kujitathmini je! kila baada ya dakika 15 umefanya nini. Usijipe mwanya, usikubali kuchelewa.

4. Nidhamu ya kufanya kazi kwa bidii / deligent / hard working.

* Hakuna sehemu nzuri ya kufanikiwa kama Tanzania kwa sababu watu wengi ni wavivu, watu wengi sio wabunifu (wana-copy na ku-paste).
* Ukifanya kazi kwa masaa ya kawaida utakuwa na maisha ya kawaida, ukifanya kazi kwa masaa yasiyo ya kawaida utakuwa na maisha ya juu zaidi / yasiyo ya kawaida.
* Kama unapenda starehe, fanya kazi kwa nguvu zaidi kuliko mtu yeyote yule.

5. Nidhamu ya kujitunza kiafya.

6. Nidhamu ya kuweka akiba na kuwekeza.

* Kama huwezi kujiwekea akiba mara kwa mara basi uwezo wa ukubwa haupo ndani yako.
* Kuwekeza ni suala la kuwa na miradi.
* Kuwekeza ni kutumia baadhi ya vitu / kitu ulicho nacho kutengeneza mkondo mwingine wa fedha.
* Ukitaka kuwa maskini tumia fedha zote ulizo nazo na ziada kidogo, fedha ambayo huipangilii itaondoka.

7. Nidhamu ya ujasiri / ushujaa / courage.

* Kila mtu duniani anaogopa kitu fulani, Lakini watu ambao wanapanda juu ni wale wanaoishinda hofu / woga. Kuna hofu ya kweli na isiyo ya kweli.
* Jaribu kuzishinda hofu zako, usipozishinda maisha yako yatabaki pale pale.
* Ujasiri unakufanya uwe na uwezo wa kumiliki mambo makubwa / biashara kubwa.

8. Nidhamu ya kujifunza endelevu / continuous learning.

* Kama kuna udhaifu Tanzania ni udhaifu wa kutopenda kujifunza.
* Mtu yeyote ambaye hana tabia ya kusoma ni sawa na mtu ambaye hajui kusoma.
* Nidhamu ya kujifunza ni Elimu binafsi.

Hivyo ndivyo James Mwang'amba alivyohitimisha; kumbuka haya niliyokueleza ni dondoo fupi tu ya kile alichozungumza. Kupata yote kwa ukamilifu wake unaombwa ufike Nchi Ya Ahadi, Sinza Kamanyola; DSM ni mbele kidogo ya KING's PALACE HOTEL.

TIMOTHY KYARA NAYE ALIACHILIA NONDO ZA UKWELI SANJARI NA DADA ABELLA BATEYUNGA (MZALENDO)


Mch. Timothy Kyara. Alizungumza vitu vingi sana vya msingi kuhusu ''JINSI YA KUJENGA NIDHAMU''.
Katika jinsi ya kujenga nidhamu, Timothy alizungumza mambo makuu matatu ya msingi.





1. Ni lazima ujue / ufahamu unataka kufanya nini.
2. Nini kitatokea kama sitafikia lengo
3. Angalia dalili.
Kupata kwa ukamilifu wake usikose jumapili ijayo tar. 27.







Mzalendo, Abella naye aliachilia nondo za kupona mtu.

Akasema, NIDHAMU NI UHURU.

Alizungumza kwa marefu na mapana ' JINSI YA KUTENGENEZA NIDHAMU YA ROHO '

Ukitaka kujua mengi zaidi, Karibu Nchi Ya Ahadi, Sinza.














Pia tarehe 26 ya mwezi huu ndani ya Nchi Ya Ahadi kutakuwa na mafunzo ya jinsi ya kutengeneza bidhaa kama vile mkaa wa makaratasi, sabuni za miche n.k.
NB: Mafunzo haya yatatolewa bureeeeeee! Ni kuanzia saa nne za asubuhi; USIKOSE.





Ndani ya Nchi Ya Ahadi utaweza kujipatia kitabu kizuri sana kilichobadilisha maisha ya watu wengi duniani na kuwa matajiri. Njoo na kiasi kidogo cha TSH. 10,000/= upate nakala yako ''MTU TAJIRI BABELI''





Endelea kutembelea blog hii, pia utapata ratiba nzima ya Ibada zinazofanyika NCHI YA AHADI.

Long Live Nchi Ya Ahadi Ministry!

KUMBUKA: 
Kama ambavyo Blog hii imekuwa ikikuletea mafundisho yenye kubadilisha ufahamu/akili na maisha kwa ujumla; Unaweza kui-support Blog hii kwa kununua mafuta halisi ya alizeti yenyo ubora wa juu, Lengo ni kufanikisha Blog hii Iendelee kukuletea mafundisho mazuri kutoka kwa watu maarufu na waliofanikiwa ambao nimekuwa nao bega kwa bega ili kuhakikisha msomaji wangu anapata kitu kitakachoweza kumtoa hatua moja kwenda hatua nyingine!
   Ili kujipatia Mafuta haya waweza kuwasiliana nasi kwa  0659 700 002 na Mungu atakubariki.
Asanteni sana wadau wangu! 


HJ




Hakikisha unaacha Comment au maoni yako hapo chini baada ya kumaliza kusoma! Maoni yako yana thamani kwetu na kwa yeyote anayepitia blog hii.

Barikiwa.

Also visit my-zone-solution finder, click here


Mawasiliano:

+255 659 700 002 / 756 145 417

mdeejunior@gmail.com


mdee.junior (skype)


@mdee_junior (twitter)



Dream Big As You Grow Big.


























Juu