Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

NITA-SUPPORT GOSPEL HIP HOP - Asema Rev. RON SWAI Ndani Ya Gospel Exclusive Interview Platform_ The GEIP.

NITA-SUPPORT MUZIKI WA GOSPEL HIP HOP - Asema Rev. Ron Swai wa kanisa la DAR CALVARY TEMPLE lililopo Tabata Shule:
Hapa akiwa ndani ya EXCLUSIVE YA: GEIP inayomilikiwa na Blogger (mdeejunior.blogspot.com) ambaye pia ni Admin wa ''GOSPEL EXCLUSIVE INTERVIEW PLATFORM''._ https://www.facebook.com/exclusive.interview Click uweze Ku-LIKE Page Yetu.


MH. FREDRICK T. SUMAYE AZUNGUMZA NA VIJANA WA KITANZANIA NDANI YA CHIMBO - SCHOOL OF THOUGHT.


Waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Mh. Fredrick Sumaye siku ya Jumapili ya tarehe 11/8/2013 alikuwa mzungumzaji ndani ya CHIMBO - School Of Thought iliyo chini ya Harris Kapiga ambaye ni Mchungaji, MC na Mtangazaji wa CLOUDS TV na CLOUDS FM Radio ya jijini Dar es Salaam.

Chimbo-School Of Thought hufanyika kila siku za Jumapili kuanzia saa 9:00 Alasiri Hadi saa 1:00 Usiku, Mahali ni Sinza Nchi Ya Ahadi (zamani kamanyola).
Mh. Sumaye alizungumza na umati mkubwa wa vijana waliohudhuria siku hiyo juu ya jinsi na namna ya kuitunza amani ya Tanzania kwa ajili yetu na kizazi kijacho baada yetu.

HIKI NDICHO ALICHOSEMA MH. SUMAYE.

Mh. Fredrick Sumaye alifunguka kwa kuonyesha uzalendo wake na mapenzi yake kwa nchi ya Tanzania ambapo hakuzungumzia chama chochote cha siasa pamoja na kuwa yeye ni mwanachama wa chama fulani kikubwa hapa nchini.

Mh. Sumaye alisema:
Amani ya Tanzania inaletwa na itatunzwa na sisi wenyewe, unajua tunaitumia siasa vibaya. Lazima sisi kama viongozi wa siasa tunatakiwa tuwe makini sana kama kweli tunataka amani iendelee kuwepo. Na umakini wetu lazima haki ionekane inatendeka ipasavyo.
Lazima vyama vya siasa viwe makini, wote tufuate sheria, tume ya uchaguzi iwe muelekezi mkuu wa taratibu za uchaguzi na tusitumie vijana kuvuruga au kuwapambanisha.

Aidha aliendelea kusema kuwa:
Zipo dalili mbalimbali za vyama vya siasa kuanzisha majeshi na hilo ni jambo la hatari litakalovuruga amani yetu kama sio kuipoteza kabisa - alisisitiza.

Katika hotuba yake, Mh. Sumaye alionekana kuongea kwa hisia sana na kuwasihi umati mkubwa wa vijana waliojitokeza kuwa makini maana wao ndio wanaotumika kwa sababu wana nguvu na rahisi kuchochewa. ''Lakini mkiwa makini hamtatumika kuchochea vurugu/fujo''-alisema kwa msisitizo.
Endapo mtakubali kutumika na kuchochea fujo/vurugu mtambue kwa hakika kuwa hizo fujo na vurugu mtakuwa nazo ninyi kwa muda mrefu kuliko mtu mwingine yeyote akimaanisha kizazi hiki na kile kijacho baada ya hiki.

Kwa hiyo kama tunataka kurithisha amani hii kwa wenzetu wanaokuja huko baada ya sisi na baada na ninyi (vijana) na vizazi vingine ni lazima tufuate taratibu nzuri za siasa.

*****************************************************************************

Click hapa uweze ku-LIKE Ukurasa wetu wa CHIMBO-SCHOOL OF THOUGHT

Jumapili hii ya Tarehe 18/8/2013 Mh. Jerry Slaa atazungumza ndani ya Chimbo-School Of Thought
mada atakayozungumza ni ''JINSI GANI UNAWEZA KUIISHI NDOTO YAKO'' How to Live your Dream.






MH. SUMAYE AKIWA AMEPIGA PICHA YA PAMOJA NA CHIMBO DIRECTORS

Wasiliana na Blog hii:
0659 700 002
0653 100 100
halisitz@gmail.com

JINSI GANI MTANZANIA ANAWEZA KUJIAJIRI - BENSON MAHENYA AZUNGUMZA NA VIJANA NDANI YA CHIMBO ''SCHOOL OF THOUGHT''






Benson Mahenya: Mmiliki wa Kampuni ya BM PUBLISHERS wachapishaji wa Gazeti La ''Afya Tabibu''











Alianza kwa kusema hivi: 

Ipo kauli isemayo kuwa ''Furaha ya mtu hujitengenezea mwenyewe'' hivyo kufikiri, kuona na kufanya ulichozaliwa nacho ni furaha kubwa sana. Inawezekana tafakuri na fikra zako umetumia muda mwingi na mlango huo uuonao bado ni mlango ambao huoni mpenyo wa kupita lakini ukiuamini na kuchukua hatua kuingia ndani hakika ipo milango mingine saba wazi inakusubiri. Daima elewa kuwa kungoja kwako kunaufanya mlango huo wa kupitia kufungwa. Ili uweze kufika sehemu fulani lazima ukutane na mtu sahihi kwani msaada wako utapatikana pale utakapochukua hatua ya kuanza. Daima mabadiliko huja baada ya kuanza.

Dondoo Muhimu.
kuanza...
kila kitu kilianza...
dunia imekuwako kwa kuanza...
mimi na wewe tuna mwanzo...

Hakika mwanzo tufe ni mvutano.

 MTAZAMO WA BIASHARA TANZANIA.

Mtazamo ni kitendo cha kulielewa jambo na kuuona mwelekeo wake katika ufahamu wa taarifa zake. Pia tunaweza kusema kuwa ni ujenzi wa mawazo juu ya jambo, tukio ama kitu halisi kilichopo au kilichopo katika ulimwengu bwete (kifikra). Hivyo mawazo yako au mtazamo wako juu ya jambo fulani daima haulingani na mtu mwingine.
Amua maisha yako mwenyewe pasipo kusubiri mtu akuamulie. 
Kwa mfano mimi mwenyewe (Benson Mahenya) nilipotaka kujiajiri nilipata vipingamizi sana na kipingamizi kikuu kilikuwa ni familia yangu ikizingatiwa ni kijana wa kwanza kati ya watoto kumi na sita yenye baba mmoja lakini mama tofauti tofauti. Hivyo mshahara wangu wa kwanza na mingine nilikuwa naituma nyumbani kusaidia ndugu zangu nikifikiri kuwa itakuwa suluhisho la matatizo yaliyowakabili ndugu zangu, lakini kumbe ndivyo nilivyozidi kuchelewa kufikisha ndoto zangu. Lakini nilipotambua kuwa yanipasa nijikwamue kwanza mimi kisha wao (ndugu). Niliwekeza katika ndoto zangu hakika sasa nimewaajiri ndugu zangu.

Kwa mtazamo wa kibiashara nchini ni vema kuweza kujua msingi wa mtazamo ambao ni Biashara. Pasipo kujua msingi wa biashara ni vigumu pia kuelewa fursa zake katika kuzifanyia kazi.

Awali ya yote tujue dhana fafanuzi ya neno biashara.
Zipo fasiri nyingi juu ya neno biashara zikiwemo;
Biashara ni kitendo cha kuuza na kununua bidhaa na huduma kulenga faida. Hii ina maana kuwa biashara yoyote lazima ilete faida ama ilenge kuleta faida. 
Unapojihusisha na biashara weka msingi mzuri wenye tija na manufaa utakaokuingizia faida.

Ujasiriamali kwa sasa ndilo neno lenye kusikika masikioni mwa watu wengi sana kwa sasa.
* Ujasiriamali ni shughuli endelevu kupata faida.
* Fasiri nyingine ni kwamba, ni kuona fursa na kuitumia.
* Ni kuona fursa, kuifuata kwa ujasiri na kuitekeleza.
Kuonekana ni neno lisilosikika tena bali ni vitu viwili vyenye mwingiliano mmoja _ UJASIRIAMALI.

VITU VYA MSINGI KATIKA KUFANYA UJASIRIAMALI NA BIASHARA.

Yajue malengo yako:
Katika ujasiriamali na biashara kwa ujumla ni vema kutambua malengo yako. Pasipo kutambua malengo ni kikwazo cha mafanikio na kusonga mbele kwa biashara.
Malengo huwekwa na mhusika mwenyewe wa biashara ama mjasiriamali. Ukiwa mjasiriamali malengo yako ni lazima yatazame kufanikisha kupatikana pesa.

Katika suala la biashara na ujasiriamali pesa ni suala muhimu kwani laweza kusimama na kuchangia kwa sehemu kubwa.
Kuhusiana na suala la pesa ni vyema ukajua malengo yako na kutaka uzifanyie nini. Katika kulenga pesa elewa utazitumia kwa ajili gani na matumizi yapi yatafanyika kukupeleka mbele au kusonga na kupiga hatua zaidi.

Unapolenga pesa katika kuzihitaji usiiangalie pesa bali kufikia malengo yako. Mfano kusomesha watoto, kupanua mradi wako.
Ukiwa mfanyabiashara mwenye mtazamo wa kusonga mbele hakikisha biashara yako inakupa faida. Boresha biashara yako upate faida kubwa. Ubunifu wenye ubora utakupa faida yenye manufaa katika biashara yako. Jenga tabia ya kufanya marekebisho yenye kuboresha biashara yako ili uwe na soko la uhakika.

Faida yaweza kuwa kubwa au kuwa nzuri kukufanikisha haraka na muda mwingine yaweza kuwa ndogo ikakufanikisha pia. Biashara yenye faida wakati mwingine yaweza kuanza pasipo faida ila itategemea uendeshwaji wake ikatoa faida na kujengeka vyema.

Mfano:
Mwanzoni mwa miaka ya 1980 siku moja katika sherehe za maonesho ya saba saba mkoani Dar es salaam, katika ufunguzi wa maonesho hayo kulikuwa na mabanda ya ujasiriamali mbalimbali likiwemo na banda la ndugu Reginald Mengi ambalo lilikuwa ni banda lililotembelewa na rais wa awamu ya kwanza hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambapo mwalimu alikutana na biashara ya maji ambayo yalikuwa yanauzwa hakika alishangazwa mno, unajua kwa nini? Wakati ule maji ya kunywa katika chupa hayakuwa na soko Tanzania kama wakati huu. Hivyo, hata faida yake haikuwa kubwa lakini hakukata tamaa hadi leo hii anaendelea.

Hivyo katika biashara suala la faida yawezekana kabisa biashara yako unapata faida ndogo usihofu maana yawezekana kabisa kesho Taifa litakutegemea kupitia hiyo biashara yako. Kataa kabisa kukata tamaa bali bidii iwe ndio msingi wa mambo yako. Ni vyema ukaitazama biashara yako kwa mtazamo wa kijasiriamali.

UJASIRIAMALI NI NINI?  Suala la biashara kupata faida ni muhimu kulitazama katika muonekano wa ujasiriamali.

Katika suala la faida si bei kubwa ndio itakupa faida bali biashara yenye mzunguko ndio itakuingizia faida.
Watu wengi wameanzisha biashara nyingi sana na nzuri lakini kukosa walengwa wa faida imesababisha biashara zao kutoendelea.
Katika mtazamo huu wa faida haikatazwi kuuza vitu vya bei ya juu bali lenga vyema faida itakayokupa mzunguko wa biashara yako.

   Kwa upande wa huduma pia, faida itazamwe vyema kwa mfano:
   Kuna huduma nyingi sana zina faida sana lakini jinsi ya kulenga kupata faida huduma hizo zimesababisha kuzorota na kutoendelea kabisa. Mfano... ''Kuna vituo fulani vya afya katika tafiti ambazo niliwahi kufanya eneo fulani kila hatua mgonjwa anayopita kutibiwa anatozwa hela. Kuandikisha majina unalipia fomu, kuonana na daktari unalipia hela, kuchukua vipimo unalipia hela, tena ni maeneo ya watu wa hali ya chini kabisa wakiwa ni wakulima pekee. Hii ilipelekea wateja kukosekana kwani faida ililengwa zaidi.
Kwa ushauri wangu (Benson Mahenya) faida ni vema iwepo lakini itakayokuza biashara. Mara nyingi unapoanza biashara anza na gharama yenye kulenga faida kidogo. Ikijulikana gharama yaweza kupanda kidogo.

Suala la faida katika biashara ni vema litazamwe vyema kwani laweza kukuza biashara ama kuiangusha. Ni vema faida ikapewa kipaumbele cha kuboreshea mazingira ya biashara ili iweze kukua.

ZINGATIA HAYA JUU YA PESA ZAKO.
> Katika suala la pesa na malengo yako, jitahidi kuiheshimu pesa ya biashara au jaribu kuitofautisha kabisa 
   na pesa ya matumizi hasa starehe.
> Usiingie mkopo hela ya biashara kununua vipodozi, kustarehe na kufanyia anasa.
   Tafuta chanzo kingine cha pesa kufanyia hivyo si biashara kwani mkopo utakugharimu.
> Pesa ya biashara iwe ndio msingi wa hatua nyingine ya kukutangaza kwenye soko. Jinsi utakavyoiheshimu,
   itakuheshimu na kukupa heshima, wengine hudai pesa yaweza kukukalisha na yeyote na kusikilizwa na
   yeyote.

> Pesa ni sabuni ya roho, yaweza kuleta kicheko japo simanzi imewazunguka wengi.
> Jitahidi kutunza/kuwekeza zaidi kuliko kutumia. Matumizi yako yasizidi kipato chako.
> Usidharau pesa ndogo kwani ndio iletayo pesa kubwa na nyingi.
> Punguza matumizi yasiyo ya lazima kwenye mzunguko wako, mfano:

* Sio kila kitu cha kununua na kula
* Zima taa ukimaliza shughuli zako nyumbani
* Zima vifaa vyote vinavyotumia umeme ofisini kwako.
* Usiendeshe gari unaongea na simu kwani waweza pata ajali ikakupa matumizi mengine.
* Zingatia usalama barabarani kuepuka kupigwa faini, mfano kuendesha gari kwa kasi, kuendesha kwa
   uzembe na kuchelewa kuamka.
* Punguza safari za kusalimia kila mtu kwani waweza pata matumizi usiyotarajia, mfano: kuchangia
   chakula kwa kuwanunulia rafiki zake mpenzi wako kwa kutokupanga (kuhonga ili kuficha aibu)
> Pesa yako ya biashara isikufanye ukaidharau ndoa yako hasa kwa wana ndoa waliofanikiwa kwa 
   kuanzia hali duni. Mmoja akifanikiwa iwe ni biashara sio kumnyanyasa mwingine. Waweza sababisha
   talaka itakayowatesa watoto.

*************************************************************************

Tuwasiliane kwa:
0659 700 002
halisitz@gmail.com


MWISHO: 
Kama ambavyo Blog hii imekuwa ikikuletea mafundisho yenye kubadilisha ufahamu/akili na maisha kwa ujumla; Unaweza kui-support Blog hii kwa kununua mafuta halisi ya alizeti yenyo ubora wa juu, Lengo ni kufanikisha Blog hii Iendelee kukuletea mafundisho mazuri kutoka kwa watu maarufu na waliofanikiwa ambao nimekuwa nao bega kwa bega ili kuhakikisha msomaji wangu anapata kitu kitakachoweza kumtoa hatua moja kwenda hatua nyingine!
   Ili kujipatia Mafuta haya waweza kuwasiliana nasi kwa  0659 700 002 na Mungu atakubariki.
Asanteni sana wadau wangu! 




  


TOFAUTI ZA KIJINSIA NA JINSI ZINAVYOATHIRI MAHUSIANO YETU_Chris Mauki





Mwanasaikolojia Chris Mauki azungumza ndani ya Nchi Ya Ahadi jinsi tofauti za kijinsia zinavyoweza kuathiri mahusiano yetu.



 
 Ni vema ukifahamu, Tunavutiwa na vitu tofauti 
Inawezekana sana mwanaume kwa jinsi alivyoumbwa akakupenda siku ya kwanza kwa mengi yale yaliyo nje yako, yeye anajua nini kimemvutia kwako na taratibu mkikubaliana kupendana ndio anaanza kugundua na kuvumbua vilivyofichwa ndani yako na hivyo ndivyo vinamfanya aidha kukukimbia au kugandana na wewe.
Lakini ni vema sana wanaume kujua kuwa siku ya kwanza mwanamke anakuona anavutiwa zaidi na “qualities” zilizoko ndani yako, sio sana vile vilivyoko nje yako. Kwahiyo ongeza juhudi katika kujenga vilivyo ndani yako kwasababu vinamashiko sana katika mahusiano yako kuliko kupoteza muda kujenga vilivyo nje yako wakati havina tija. Ni sawasawa na kutumia nguvu ngingi kutengeneza mtego wa kunasa nguruwe pori huku ukiwa na nia ya kwenda kutega kware.
Siku zote dhana ya mahusiano inaweza kuwa na namna mbili tofauti kutokana na tofauti za jinsia zetu wenyewe. Lakini kwanza tujiulize nini maana ya MAHUSIANO?

Mahusiano_ Ni ujenzi wa uhusiano wa kijinsia kati ya mwanaume na mwanamke unaohusisha sana hisia.

TUNAWEZA KUYAGAWANYA MAHUSIANO KATIKA MAKUNDI MANNE.

1> Kundi la watu walio katika mahusiano ya urafiki hadi uchumba.
2> Kundi la watu wanaoanza kujiunga/kujiingiza kwenye mahusiano.
3> Kundi la watu ambao tayari wako kwenye ndoa.
4> Kundi la watu ambao hawajajiingiza kwenye mahusiano kabisa.

TOFAUTI ZA KIJINSIA.

Mara nyingi kunaweza kuwa na tofauti mbalimbali kutokana na utofauti wa kijinsia unaotokana na chanzo au vyanzo mbalimbali vinavyoleta tofauti ambayo inatokana na Asili Yetu.
Asili yetu ni pale mmoja asemapo ''mimi ni mwanaume, yeye ni mwanamke''

VYANZO VYA TOFAUTI HIZI.

a) Malezi. 
Mara nyingi malezi ndiyo yanayoweza kuonyesha tabia asilia ambayo anayo mtu kulingana na jinsia yake. Wazazi ndio nyenzo kuu ya kumfanikisha mtoto kuwa na malezi bora yenye mtazamo mzuri wa kuwa na mahusiano mazuri kwa wazazi wenyewe na hata kwa jamii inayomzunguka.
Lazima wazazi watumie vyema fursa zao kuwajenga watoto wao katika misingi iliyo thabiti katika maisha yao yote.

b) Makuzi.
Katika hatua ya ukuaji mzazi ndiye amtengenezaye mtoto katika hatua zote za ukuaji wa kimwili na kiroho kutokana na umri wake.

Utafiti alioufanya Chris Mauki.

Katika utafiti wangu ( Chris Mauki), 2012 huko Afrika Ya Kusini imeonyesha kuwa familia nyingi huwa na mzazi mmoja (single parent family) ambapo watoto huwa chini ya uangalizi wa malezi ya mzazi mmoja, hivyo mtoto huathiriwa kisaikolojia zaidi.

Mfumo/aina za familia:
Familia ni mkusanyiko wa watu wenye uhusiano mmoja na kukaa pamoja.

Aina za familia.
-familia yenye mzazi mmoja na watoto (single parent family)
-familia yenye wazazi wawili (nuclear family)
-familia yenye wazazi, watoto na ndugu wengine (extended family)
-familia ambayo haina wazazi (non-parents family)

c) Watu wanaokuzunguka (marafiki).
Huenda marafiki au watu wanaokuzunguka ndio wanaoweza kuwa chanzo cha kuibua utofauti, kwani unaweza kusikia maneno yanayosemwa kwa kujadili mambo ambayo ni sumu kali ya kuibua tatizo katika jamii.

d) Maisha yako ya awali (life background).
Ujionavyo nafsini mwako ndivyo ulivyo na ndivyo watu watakavyokuona. Maisha yako ya awali yanaweza kukupa swali la kujiuliza; 'jinsi ujionavyo nafsini mwako ndiyo chimbuko la kuibua furaha au huzuni maishani mwako'.

Matatizo ya kimahusiano:
Matatizo siku zote hutokana na namna mtu anavyoweza kujitengenezea mwenyewe.
Lakini matatizo ya kimahusiano watu wengi hushindwa kuyatatua kwa sababu ya kutokujua tofauti zao za kijinsia.

Mifano ya tofauti za kijinsia.
i> Wanawake wengi wameathiriwa na manunuzi (shopping) wakati wanaume hawazingatii sana manunuzi/shopping.

ii> Wanawake wengi hawazingatii sana mpangilio wa muda katika mipango yao. Lakini wanaume wengi huzingatia muda zaidi.

iii> Kwa matumizi ya pesa wanawake hutumia vibaya kuliko wanaume.

Nini tufanye kutatua tatizo?

- Lazima kila mtu aelewe chanzo cha tatizo na kulitatua
- Utayari wa kuchukuliana udhaifu
- Kuendana tabia.

JE! WANAWAKE WANASEMA NINI KWA WANAUME?
Kwa tafiti zilizofanywa nchini, imeonekana kuwa wanaume hawawezi kuelezea hisia zao walizo nazo kwa undani zaidi.

Wanaume pia hawana ukweli katika kuonyesha uhusiano zaidi.

Wanaume wengi wana fikra hasi kwa wanawake.

######################################################################

HAKIKA UHUSIANO BORA HUIBUA FURAHA MAISHA YOTE.


MWISHO: 
Kama ambavyo Blog hii imekuwa ikikuletea mafundisho yenye kubadilisha ufahamu/akili na maisha kwa ujumla; Unaweza kui-support Blog hii kwa kununua mafuta halisi ya alizeti yenyo ubora wa juu, Lengo ni kufanikisha Blog hii Iendelee kukuletea mafundisho mazuri kutoka kwa watu maarufu na waliofanikiwa ambao nimekuwa nao bega kwa bega ili kuhakikisha msomaji wangu anapata kitu kitakachoweza kumtoa hatua moja kwenda hatua nyingine!
   Ili kujipatia Mafuta haya waweza kuwasiliana nasi kwa  0659 700 002 na Mungu atakubariki.
Asanteni sana wadau wangu! 









Juu