Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

HATIMAYE CHRIS MAUKI AJA KIVINGINE! KIVIPI - TWENDE PAMOJA!

 




CHRIS MAUKI ni Mhadhiri Msaidizi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam aliyebobea katika ‘Saikolojia ya Kijamii na Ushauri Nasaha’. Kwa sasa Chris anafanya masomo yake ya Shahada ya Uzamivu Pretoria, Afrika Ya Kusini katika masuala ya ‘Maamuzi na Matokeo Ya Talaka’ – (matokeo hayo kwa watoto). Chris amekuwa ni baraka kwa jamii ya kitanzania kupitia vitabu, semina na vipindi mbalimbali vya redio na TV ambavyo ameandika na kufanya.

Siku ya jana 02/02/2014 Chris alifunua siri ya mafanikio  na jinsi ya kuandaa mazingira yatakayoleta au sababisha mafanikio hayo.
Chris alianza kwa kusema hivi:
Kuna vitu vingi ambavyo unaweza kuvipata Lakini kati ya hivyo kuna kimoja ambacho huwezi kukisahau. Wengi tunataka kufanikiwa na tunasoma vitabu vya mafanikio na bahati mbaya Watanzania tunataka mafanikio ya haraka. Kwa hiyo watu wanatamani mafanikio tena ya haraka haraka.

Siku hizi kila kitu ni haraka na ndio maana watapeliwa ni wengi sana. Anayetapeliwa ni kwa sababu anataka au anatamani kupata fedha za haraka.
* Hata wasioongea mafanikio wanatamani mafanikio.
* Na wapo ambao wanaomgea mafanikio ya wengine.

NINI TAFSIRI YA MAFANIKIO / MAFANIKIO NI NINI?

Tofauti ya mafanikio inatokana na tafsiri ya mafanikio.
Mafanikio ni process / mchakato
Utajua mtu fulani kafanikiwa kulingana na tafsiri ya mafanikio.
* Mafanikio yasiyo na maelezo ni tatizo, na mafanikio ya namna aina hiyo lazima kuna Injustice/dhuluma/mapato yasiyo ya haki.
* Dunia ya sasa watu wanataka mafanikio bila process / mchakato.

Mafanikio yanategemeza mchakato mzima wa matendo kuyaendea maafanikio.

TAFSIRI:
Tafsiri ya mafanikio iliyopo ni ''UWEZO WA KUMILIKI'' hii ni tafsiri au mtazamo usio sahihi.
* Ukiingia kwenye mahusiano kwa tafsiri hii utajikuta unaingia kwa speed 100 lakini mwisho wa siku utatoka kwa speed 200, na utaumia.

TAFSIRI / MTAZAMO SAHIHI.
Ni mafanikio ya Ujumla - Well being, yaani ujumla wa utu wa mtu, hali ya kiroho, afya, mahusiano, vile macho yanaweza kuona na vile macho hayawezi kuona. Ni uwiano wa vile vinavyo onekana na vile visivyo onekana.

NJIA ZA KUJITENGENEZEA MAZINGIRA YA MAFANIKIO BINAFSI:

Mafanikio huenda kwa wale walioandaa mazingira ya kufanikiwa. Kwa hiyo mafanikio yanafananishwa na maji ya mvua.
* Tanzania tunaongoza kwa uvivu wa kufikiri
* Uvivu wa kufikiri huleta uvivu wa kutenda

1. Elewa umuhimu wa muda na jifunze kuukomboa
* Kuna tofauti ya kutunza muda na kuukomboa muda ( save time vs redeem time), you can save money but you can't save time. Hata usipoutumia muda utaenda tu!
To redeem means to use effectively / kukomboa muda ni kuutumia muda kiufanisi/kikamilifu bila kuupoteza.
* Epuka kufikiri kuwa una muda, hata kwenye maandiko matakatifu shetani ameambiwa kuwa ana muda mchache na anajua hivyo. Don't buy excuses!

2. Jifunze kujiwekea malengo na kuyafikia
Lengo ambalo hujalioaanisha/hujalihusianisha na muda hubaki kuwa ndoto 'a wish'.
Lengo ukilihusisha na muda utakuwa na focus.

AINA MBILI ZA MALENGO.
Kuna aina mbili za malengo. i>. Malengo ya muda mfupi (short term plan), kama mwaka mmoja hivi.
ii>. Malengo ya muda mrefu (long term plan), kuanzia miaka miwili hivi.
Hivyo usipojua lengo lako ni lipi itakupa shida.

Ili malengo ya muda mrefu yafanikiwe lazima malengo ya muda mfupi yawe yamefanikiwa. Usipofikia pale unatamani kufikia, itabaki kuwa ndoto. Ili ndoto ifikie kwenye uhalisia ''reality'' lazima uiwekee mikakati/malengo.
Ukishindwa kuweka malengo utaishia kuota ndoto.

3. Weka malengo yako kwenye akili.

4. Weka malengo yako moyoni - ili uweze kuyakumbuka kisha yaandike mahali / documentation.
Kisaikolojia, kuna uwezo mkubwa sana wa kukumbuka kitu ulichoandika kuliko usichokiandika.

5. Jifunze kupambana / fight. Pia uwe macho - don't loose focus!

MASWALI MATATU YA KUJIULIZA:
(a) Unataka nini maishani au kwenye malengo yako?
(b) Utatumia mbinu gani kufikia hilo lengo?
(c) Utatumia rasilimali gani - 'resources' kufikia malengo yako?

Sio kila mtu anaweza au anafaa kukufikisha kwenye lengo, mnaweza kuanza pamoja lakini msifike pamoja.
Hivyo basi, kama lengo lako ni kufanikiwa maishani uwe macho unaoa au unaolewa na nani.

UMUHIMU WA KUWEKA MALENGO
1. Malengo yanatusaidia sana kuweza kufikia tulichokipanga.
2. Malengo yanatusaidia kufahamu uwezo wetu (potentiality).
3. Malengo yanatusaidia kuweka kipaumbele ''focus'' kwenye matokeo, itakusaidia kutokuwa  - busy for nothing.

UNAWEZAJE KUKOMBOA MUDA.

1. Fahamu wewe ni mtu wa aina gani ( yaani uwezo wako wa kufanya vizuri ni asubuhi, mchana au usiku)
2. Elewa ni vitu gani vinakupotezea muda
3. Tofautisha kati ya muda bora na kazi bora
4. Kula vizuri - eat well (balanced diet). Uwezo wa kufikiri unategemezwa zaidi na kile unachokula.
5. Jifunze kupumzika - rest is not the waste of time.
6. Epuka kulundika kazi.
7. Tengeneza muda wako mwenyewe
8. Jifunze kusema hapana - ili ufanye mambo muhimu au upumzike.

KATI YA JANGA KUBWA KABISA DUNIANI SIO KIFO  BALI NI MAISHA YASIYO NA MALENGO.

Contacts:
0659 700 002
0756 145 417
0653 100 100 

MWISHO: 
Kama ambavyo Blog hii imekuwa ikikuletea mafundisho yenye kubadilisha ufahamu/akili na maisha kwa ujumla; Unaweza kui-support Blog hii kwa kununua mafuta halisi ya alizeti yenyo ubora wa juu, Lengo ni kufanikisha Blog hii Iendelee kukuletea mafundisho mazuri kutoka kwa watu maarufu na waliofanikiwa ambao nimekuwa nao bega kwa bega ili kuhakikisha msomaji wangu anapata kitu kitakachoweza kumtoa hatua moja kwenda hatua nyingine!
   Ili kujipatia Mafuta haya waweza kuwasiliana nasi kwa  0659 700 002 na Mungu atakubariki.
Asanteni sana wadau wangu! 





 

TAMBUA MISSION YAKO PALE ULIPO - By Apostle Mdee Junior!


Tunaendelea na mfululizo wetu wa segment ya ''DRAW ME CLOSE''
Leo tutajifunza kitu kutoka kitabu cha Yohana Mtakatifu Sura yote ya nne(4)

Mahali popote ulipo au unapopitia lazima ujue mission yako ni nini katika hilo jambo au mahali ulipo.

Tazama video hii kwa kubofya kitufe cha ''Play'' usikie kile mtumishi wa Mungu Apostle Mdee Junior anasema nawe leo kupitia neno la MUNGU.

Ukishamaliza kutazama hiyo video usisahau kutupia comments zako hapo chini au tufuate kwenye ukurasa wetu wa facebook: https://www.facebook.com/draw.close

Karibu tujifunze.

Mawasiliano: 0659 700 002




NAWASHUKURU WASOMAJI WANGU, SASA TUMEFIKIA WASOMAJI ZAIDI YA ELFU 29,000.ENDELEA KUWASHIRIKISHA NA WENGINE.

JITAMBUE SAIKOLOJIA: DONDOO ZA MSINGI KWA WALIOKO KWENYE MAHUSIANO - Part 4.


KATIKA MAHUSIANO:

Kwa kadiri ambavyo wapenzi wakike wanazidi kurusha lawama, kulalamika na kuwa wapinzani, ndivyo ambavyo wapenzi wao wa kiume wanazidi kujikwepa nao, kujiepusha nao, na kujitahidi kuwanyamazia. Kwa kadiri ambayo wapenzi wakiume wanaendelea kujikwepa, kujiepusha na kuwanyamazia wapenzi wao wakike ndivyo pia ambavyo wapenzi wakike huzidi maradufu kulalamika, kulaumu na kuwa wapinzani, “Crazy cycle”. Kama mzunguko huu usiposhuhulikiwa na kuvunjwa mapema tena kwa busara basi mahusiano yenu yanaweza kabisa kuishia kwenye ganzi (mnaishi na mwenzako tu kama mpangaji mwenza na sio “soul mate”) au yanaweza ishia kwenye talaka. Na kwa hali hii ukisikia mwenzako ana “cheat” wala usihamaki na ku ‘panic” kwasababu hapa ndiko mbegu ya “cheating” inawekewa mbolea, nafahamu kabisa uliyeko kwenye hii “cycle” unaelewa ninazungumza nini.

Sio marazote wapenzi wetu wa kike wanapokinzana na sisi, kutupayukia, kukwaruzana na kuwa wabishi wanamaanisha hawana heshima kwetu, wanatudharau, wanatabia mbaya na labda hawajakuzwa vema, la hasha! Mara kwa mara hiyo ni lugha ya jinsia ya kike kupaza sauti kwako kuomba umpende, umpende zaidi, umpende kama zamani. Yamkini tafsiri yako ya kumpenda inayopelekea wewe kufanya unayoyafanya ukihisi yeye naye anatafsiri ni penzi kumbe sivyo. Chukua nafasi ya kumfahamu na kufahamu tafsiri halisi aliyonayo yeye, halafu mpende kwa tafsiri ile. Unapompenda mpenzi wako kwa tafsiri ya penzi aliyonayo yeye, unampa nafasi pia yeye kukupenda kwa ile tafsiri ya penzi uliyonayo wewe. Taratibu utaona ile mikikimikiki na mikwaruzano inapungua. Mahusiano yenu yanajawa na utoshelevu wa moyo, jambo ambalo wengi wetu ni mashahidi kuwa hautilipati kwenye mahusiano yetu “NI UELEWA TU, WALA SI UCHAWI”.

Katika utafiti uliofanywa kwa wanaume 400 walio ulizwa swali kuhusu kupendwa au kuheshimiwa na wapenzi wao wakike, asilimia 74 ya wanaume walijibu "ni bora niishi na mwanamke anayeniheshimu hata kama hanipendi kuliko kuishi na mwanamke anayenipenda lakini haniheshimu". Majibu ya wanaume hawa hayamaanishi kuwa wanaume hawa hawahitaji kupendwa bali kwao penzi ni kama CHAKULA na kuheshimiwa ni kama MAJI. Wanaweza kuishi pasipo chakula lakini sio pasipo maji. Sasa hapa kazi kwako kwenye kutafuna, kumeza au kutema.

Chris Mauki.
Saikolojia Ya Jamii Na Ushauri - UDSM.

Inaendelea...
Usikose Part 5
0659 700 002
0653 100 100

NAWASHUKURU WASOMAJI WANGU, SASA TUMEFIKIA WASOMAJI ZAIDI YA ELFU 26,000. ENDELEA KUWASHIRIKISHA NA WENGINE.

JITAMBUE SAIKOLOJIA: DONDOO ZA MSINGI KWA WALIOKO KWENYE MAHUSIANO - Part 3.


KATIKA MAHUSIANO:

Suala la kutaka kuolewa au kutaka kuoa sio tu jambo la kuzungumza kwa kunuia au kutamani bali ni suala la kujitahidi “kuwa”, “it is not just a wish, but a matter of becoming”. Muda unaopoteza kutamani na kuongea tu kuhusu ndoto zako za kuoa au kuolewa ungeutumia vema katika kujitengeneza, ku “qualify” kuwa mume au mke bora. Hata kama unaongea sana na una “wish” sana na wazazi wako wana tamani sana pia kuona unaolewa au unaoa bado yote hii haikufanyi kamwe kuwa “a husband/wife material” kama bado hujaamua kuweka jitihada binafsi kuwa hivyo. Watu hawaoi mtu anayetamani kuwa mke, na hawaolewi na mtu anayetamani kuwa mume, watu wanaoa mke na wanaolewa na mume aliyeonyesha taswira ya kuwa mume au mke hata kabla hajaingia katika taasisi hiyo. Usitegemee ku “qualify” kuwa mume au mke ukishajisajili kwenye taasisi hiyo, “it will be too late” na kwa bahati mbaya wengine wetu tunaishi na wenza ambao ukimtazama kwa mtazamo yakinifu unaona bado anakazana na kujitahidi kuwa mke au mume. Kumbuka!! Mtu anakuwa rubani kwanza ndiyo anapewa “uniform” baadae, sio anapewa “uniform” kwanza halafu ndiyo akajifunze urubani, “never on earth”

Kila mara katika mahusiano yako zikabili changamoto ukiwa na mtazamo moyoni na nafsini mwako kwamba utashinda, bila kujali ushindi huo unakuja polepole kiasi gani. Kamwe usizikabili changamoto zako ukiwa umeinama moyo na kughubikwa na mtazamo wa kushindwa kwasababu nakuhakikishia "You will go down indeed".

Japokuwa wanaume wanaweza kuwa na uhakika mioyoni mwao kwamba wanapendwa na pia wanawapenda kwa dhati wapenzi wao bado huwa ngumu sana kwa wanawake kuwa na uhakika kama kweli wanapendwa na wapenzi wao.

Sio tu kwamba wanaume na wanawake huona vitu kwa mitazamo tofauti bali pia husikia mambo kwa mitazamo tofauti sana. Ujumbe uleule mmoja waweza kutafsiriwa kwa utofauti mkubwa sana na mara nyingine kuamsha mikwaruzano hususani kama hamjajipanga kuzifahamu tofauti hizi.

Chris Mauki
Saikolojia Ya Jamii Na Ushauri - UDSM.

Inaendelea...
Usikose Part 4
0659 700 002
0653 100 100 

 
NAWASHUKURU WASOMAJI WANGU, SASA TUMEFIKIA WASOMAJI ZAIDI YA ELFU 26,000. ENDELEA KUWASHIRIKISHA NA WENGINE.

Juu