Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

Unto Jesus every knee shall bow and tongue confess that He's Lord!


IT'S ALL ABOUT OVERCOMERS FM RADIO ''ON AIR NOW''!


Kituo cha radio ya Kikristo mkoani Iringa kinachojulikana kwa jina la ''Overcomers Fm Radio'' iliyo chini ya huduma ya Overcomers Power Centre inayomilikiwa na Mtumishi wa Mungu Nabii, Dr. BOAZ SOLLO, sasa matangazo yake yamerudi hewani baada ya kutokea tatizo la kiufundi lililopelekea kutosikika kwa matangazo yake hewani kwa takribani majuma mawili hivi.

Meneja masoko (marketing manager) FREDY MWAKYENDENGE wa radio hiyo alipozungumza na mwandishi/mmiliki wa Blog hii pendwa nchini na nje ya nchi alisema:
''Kwa niaba ya Uongozi wa kituo hiki cha radio nachukua nafasi hii kuomba radhi kwa wasikilizaji wote wa overcomers fm radio kwa kutokupatikana hewani kwa muda usiozidi majumaa mawili kutokana na matatizo ya kiufundi lakini sasa hivi hali imekuwa shwari na wasikilizaji waendelee kubarikiwa na vipindi vya radio yao pendwa vyenye kuelimisha, kuburudisha pamoja na kuwatoa watu kutoka katika vifungo mbali mbali vya adui shetani. Napenda kuwatangazia kwamba leo 22/7/2013 tumerudi hewani kwa mara nyingine tena''. Mwisho wa kumnukuu.

Aidha bwana Mwakyendenge alitumia nafasi hii kumshukuru mtumishi wa Mungu Nabii na Dr Boaz Sollo wa huduma ya OVERCOMERS POWER CENTRE anayefanyia ibada zake katika ukumbi wa shule ya Sekondari Togwa mkoani Iringa ambaye ndiye Mkurugenzi wa Ovecomers fm radio kwa jitihada alizozifanya katika kuhakikisha wananchi wa Iringa na maeneo ya jirani wanaendelea kubarikiwa na radio yao pendwa ya Overcomers.

BLOG HII INAWATAKIA USIKILIZI MWEMA WA 98.6 FM

AMEN!


«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:


Juu