Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO




MITHALI 24:11.

Siku ya Jumapili ya tarehe 24. March 2012, Blog hii ilikuwa maeneo ya Kongowe, Kibaha Mkoani Pwani. Nilikutana na dada mmoja ambaye aliniambia kuwa mtoto wake alimzaa akiwa salama kabisa, lakini siku moja alishangaa kuona akimkalisha mtoto chini hawezi kukaa, akimsimamisha anasimamia vidole, akashtuka. Ndipo alipoamua kumpeleka hospitali, akaambiwa mtoto ana matatizo ya kichwa kujaa maji. JINA LA MTOTO NI: EVA.

Dada huyu amehangaika sana na mtoto tangu January mwaka jana hadi leo, amezunguka kila mahali kutafuta msaada wa kunusuru maisha ya mtoto wake. Lakini sasa ameamua kumrudia Mungu na anaomba msaada wa maombi kwa ajili ya mtoto wake.
Amefungua mlango kwa mtumishi yeyote kwenda nyumbani kwake kumtembela na kufanya huduma ya maombi pamoja.

WITO:

IKIWA WEWE NI MWANAMAOMBI/MTUMISHI NA UNA HUDUMA YA USHAURI NA KUFUNGUA WALIO KATIKA VIFUNGO, NAOMBA UWASILIANE NAMI KWA NAMBA ZIFUATAZO ILI IKIWEZEKANA TUONGOZANE TUKAFANYE HUDUMA HIYO PAMOJA, NA MUNGU ATATUKUZWA.... NA WEWE UTABARIKIWA ZAIDI.



0659 700 002 / 0756 145 417.

PICHA ZINGINE.




«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:


Juu