Chat Now

HABARI MPYA

FUNDISHO LA MSINGI

PICHA NA MATUKIO

CAPACITY BUILDING CLASS

MAHUSIANO

NUKUU YA LEO

Baada ya utangulizi na kuona nini maana ya ushirika ikwa sambamba na Maandiko Matakatifu; leo napenda kukupa mwendelezo wa somo hili zuri sana.
Leo tunaingia sehemu ya pili.

NB: UNAOMBWA KUTOA MAONI YAKO KUHUSU SOMO HILI PIA JE MUNGU AMEKUHUDUMIA KWA KIASI GANI KUPITIA SOMO HILI?


















USHUHUDA WA WATU WALIOKUWA NA USHIRIKA NA ROHO MTAKATIFU.

Daniel 6:10.
Hata Daniel, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake; ( na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalem ) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.
* Daniel alikuwa na maisha ya Ushirika na Roho Mtakatifu, si kwa sababu tu ya matatizo yaliyomkabili.

Zaburi 55: 16,17.
Nami nitamwita Mungu, Na Bwana ataniokoa; Jioni, asubuhi na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.
* Ushirika na Roho Mtakatifu unatufanya kuwa waombaji, pia hutufanya tumtegemee Mungu 
   zaidi katika maisha yetu ya kila siku sanjari na kila pito tunaloweza kulipitia katika maisha yetu.

Marko 1:35.
Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.

* Yesu alikuwa na ushirika na Roho Mtakatifu
* Ushirika _ Ni urafiki
* Ushirika na Mungu ni moyo wa Mungu kuwa ndani yangu / yako; au moyo wa Mungu kuwa moyo wangu/
   wako.

1Kor. 6:17.
Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.
* Ushirika ni umoja katika roho / moyo.

Ruthu 1:1-5.
Ikawa zamani za Waamuzi walipoamua, kulikuwa na njaa katika nchi. Akaondoka mtu mmoja wa Bethlehemu ya Yuda, akaenda kukaa katika nchi ya Moabu, yeye na mkewe na wanawe wawili; Na jina la mtu huyo aliitwa Elimeleki, na jina la mkewe Naomi, na majina ya wanawe wawili Maloni na Kilioni, Waefrathi wa Bethlehemu ya Yuda. Wakafika nchi ya Moabu, wakakaa huko. Akafa Elimeleki mumewe Naomi; na yule mwanamke akasalia na wanawe wawili. Nao wakaoa wake katika wanawake wa Moabu; na jina la mmoja aliitwa Orpa, na jina la wa pili Ruthu. Wakakaa huko yapata miaka kumi. Wakafa na Maloni na Kilioni wote wawili; na huyo mwanamke akawa amefiwa na wanawe wawili, na mumewe pia.

* Siku zote Mungu anatufundisha ili tupate faida, tupate kufanikiwa.
* Ziko nyakati za njaa. Je! Unafanya nini yanapotokea hayo?


Je! unafanya nini wakati unapokuwa chini / kupungua nguvu za kiroho?
Yesu alifanya nini alipoguswa na yule mwanamke mwenye kutokwa na damu? (maana alihisi kupungukiwa nguvu).

* Wakati wa kushuka / kupunguka nguvu ndio wakati muafaka wa kuwa na ushirika na Roho Mtakatifu
* Elimeleki aliikimbia njaa - AKAFA. Hatutakiwi kukimbia.


UNAFANYA NINI NJAA INAPOINGIA? (sehemu ya tatu)   Itaendelea, Usikose!


Sikiliza wimbo huu wa Christina Shusho, Ushirika na Roho. Barikiwa!




«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:


Juu