Wednesday, April 30, 2025

Chat Now

headlines

    HABARI MPYA

    FUNDISHO LA MSINGI

    Fundisho La Msingi

    PICHA NA MATUKIO

    Picha Na Matukio

    CAPACITY BUILDING CLASS

    MAHUSIANO

    NUKUU YA LEO

    NUKUU YA LEO


    KATIKA MAHUSIANO:

    Suala la kutaka kuolewa au kutaka kuoa sio tu jambo la kuzungumza kwa kunuia au kutamani bali ni suala la kujitahidi “kuwa”, “it is not just a wish, but a matter of becoming”. Muda unaopoteza kutamani na kuongea tu kuhusu ndoto zako za kuoa au kuolewa ungeutumia vema katika kujitengeneza, ku “qualify” kuwa mume au mke bora. Hata kama unaongea sana na una “wish” sana na wazazi wako wana tamani sana pia kuona unaolewa au unaoa bado yote hii haikufanyi kamwe kuwa “a husband/wife material” kama bado hujaamua kuweka jitihada binafsi kuwa hivyo. Watu hawaoi mtu anayetamani kuwa mke, na hawaolewi na mtu anayetamani kuwa mume, watu wanaoa mke na wanaolewa na mume aliyeonyesha taswira ya kuwa mume au mke hata kabla hajaingia katika taasisi hiyo. Usitegemee ku “qualify” kuwa mume au mke ukishajisajili kwenye taasisi hiyo, “it will be too late” na kwa bahati mbaya wengine wetu tunaishi na wenza ambao ukimtazama kwa mtazamo yakinifu unaona bado anakazana na kujitahidi kuwa mke au mume. Kumbuka!! Mtu anakuwa rubani kwanza ndiyo anapewa “uniform” baadae, sio anapewa “uniform” kwanza halafu ndiyo akajifunze urubani, “never on earth”

    Kila mara katika mahusiano yako zikabili changamoto ukiwa na mtazamo moyoni na nafsini mwako kwamba utashinda, bila kujali ushindi huo unakuja polepole kiasi gani. Kamwe usizikabili changamoto zako ukiwa umeinama moyo na kughubikwa na mtazamo wa kushindwa kwasababu nakuhakikishia "You will go down indeed".

    Japokuwa wanaume wanaweza kuwa na uhakika mioyoni mwao kwamba wanapendwa na pia wanawapenda kwa dhati wapenzi wao bado huwa ngumu sana kwa wanawake kuwa na uhakika kama kweli wanapendwa na wapenzi wao.

    Sio tu kwamba wanaume na wanawake huona vitu kwa mitazamo tofauti bali pia husikia mambo kwa mitazamo tofauti sana. Ujumbe uleule mmoja waweza kutafsiriwa kwa utofauti mkubwa sana na mara nyingine kuamsha mikwaruzano hususani kama hamjajipanga kuzifahamu tofauti hizi.

    Chris Mauki
    Saikolojia Ya Jamii Na Ushauri - UDSM.

    Inaendelea...
    Usikose Part 4
    0659 700 002
    0653 100 100 

     
    NAWASHUKURU WASOMAJI WANGU, SASA TUMEFIKIA WASOMAJI ZAIDI YA ELFU 26,000. ENDELEA KUWASHIRIKISHA NA WENGINE.

    «
    Next
    JITAMBUE SAIKOLOJIA: DONDOO ZA MSINGI KWA WALIOKO KWENYE MAHUSIANO - Part 4.
    »
    Previous
    JITAMBUE SAIKOLOJIA: DONDOO ZA MSINGI KWA WALIO KWENYE MAHUSIANO - Part 2.

    No comments: